Chama
cha Wastaafu na Wazee Mkoa wa Mtwara (Chawamu) kimelalamikia wanasiasa
wanaogombea nafasi mbalimbali za uongozi kuwasahau wazee katika sera
zao.
Katibu wa chama hicho, Wilbard Nandonde, alisema chama kinashangazwa na baadhi ya wagombea wa nafasi za urais, ubunge na udiwani kutoongelea kuhusu mustakabali wa changamoto zinazowakabili wazee na badala yake kujikita kutoa ahadi katika nyanja nyingine.
Alisema waliamua kusambaza makaratasi katika vyama mbalimbali vya siasa na ofisi za serikali, ambazo zinaelezea changamoto hizo zilizoshindwa kutatuliwa kwa kipindi kirefu.
Katibu wa chama hicho, Wilbard Nandonde, alisema chama kinashangazwa na baadhi ya wagombea wa nafasi za urais, ubunge na udiwani kutoongelea kuhusu mustakabali wa changamoto zinazowakabili wazee na badala yake kujikita kutoa ahadi katika nyanja nyingine.
Alisema waliamua kusambaza makaratasi katika vyama mbalimbali vya siasa na ofisi za serikali, ambazo zinaelezea changamoto hizo zilizoshindwa kutatuliwa kwa kipindi kirefu.
Tumegawa katika ofisi zote za vyama na baadhi ya wagombea tumewapatia..sasa hayo mambo yako mengi lakini sisi tunaomba tu kwamba wazee wasitusahau katika kunadi sera zao au katika manifesto yao wawe wanatutaja sisi wazee watatufanyia nini.. alisema.
Alisema yapo mapendekezo mengi ya wazee ambayo serikali bado haijayafanyia kazi ikiwa ni pamoja na kutopitishwa kwa sera ya wazee ya mwaka 2003 kuwa sheria ambayo kwa kiasi kikubwa ingeweza kuwalinda.
Angalia toka 2013 mpaka leo ni karibu miaka 12 lakini hii sera bado haijatungiwa sheria...mambo mengine ya manyanyaso labda mtu anakutukana, kama ingekuwa sheria sisi wenyewe tungechukua hatua.
Mtu anayekutukana unamkamata na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria, lakini kwa sababu ni sera inaonekana haina mguvu yoyote.. aliongeza.
Aidha, alisema suala la kupata bure huduma za matibabu halitekelezwi na kuzitaka halmashauri zote kuandaa vitambulisho vya wazee kwa ajili ya kutambulika na kupatiwa matibabu bila kulipia gharama yoyote.
Alitoa wito kwa serikali kukomesha vitendo vya mauaji ya wazee ambavyo kwa kiasi kikubwa vimekuwa vikitokea katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, vinatokana na baadhi ya watu kuwa na imani potofu za kishirikina.
Mwanachama wa chama hicho, Erntrudis Mpokwa, aliitaka manispaa ya Mtwara Mikindani, kutoa msamaha wa kodi za majengo kwa wazee wastaafu wa manispaa hiyo ambao uwezo wao wa kipato ni mdogo na hata nguvu ya kutafuta kipato sio kubwa kiasi cha kumudu gharama ya kulipa Sh. 20,000 inayotozwa kwa mwaka.
Mchina Nnamba, alisema kodi inayotozwa na manispaa hiyo sio ya nyumba isipokuwa ni ya mtaa kwa sababu viwango vinatozwa kutokana na hadhi ya nyumba ni tofauti.
ìSasa matokeo yake hawatozi kodi ya thamani ya nyumba, ila watoza kodi ya mtaa ambayo haipo..mimi jana (juzi) nilipewa hiyo barua nikawaambia haya madai yenu ni ya mtaa na sio ya nyumba, nyumba yenye thamani hii mimi sina kwanza uiwahi kufika ukaiona hiyo nyumba?..hilo ni jambo ambalo wazee wamelalamika mara nyingi..î alisema.
Chama hicho kimejipanga kuadhimisha siku ya wazee duniani katika wilaya ya Nanyumbu mkoani hapa itakayofanyika Oktoba mosi, mwaka huu, ambapo kitaifa itaadhimishwa mkoani Kigoma.
CHANZO:
NIPASHE JUMAPILI
Sunday, September 20, 2015
Kubandika matokeo ya urais vituoni kumechelewa
Kwa namna ambavyo uamuzi wa kubandika matokeo ya kura za urais katika vituo vya kupigia kura umepokewa na wananchi, ni dhahiri kuwa huo ni uamuzi uliochelewa na ulikuwa unasubiriwa na wengi.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) juzi ilitangaza kuwa kuanzia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, matokeo ya kura za urais yatakuwa yanabandikwa kwenye vituo vya kupigia kura sambamba na yale ya ubunge na udiwani, hatua ambayo imepongezwa na wengi.
Uamuzi huo wa Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu, Damian Lubuva ulitolewa katika mkutano wa viongozi wa dini, baada ya viongozi hao kueleza wasiwasi wao katika uchaguzi huu, ikwamo kura za urais pekee kutobandikwa vituoni tofauti na zile za ubunge na udiwani.
Kwa mujibu wa Jaji Lubuva, licha ya kubandikwa vituoni, utangazaji wa matokeo husika utafanyika kama kawaida katika kila ngazi, ya udiwani kwenye kata, ubunge wilayani, lakini matokeo ya jumla ya urais yatatangazwa na makao makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Pamoja na kuwaondolea wasiwasi wananchi kuhusu usalama wa kura zao, mwenyekiti huyo wa NEC aliwahi kukaririwa na gazeti hili akisema ,“Hakutakuwa na nafasi ya kuandaa vijana kulinda kura kwa sababu kura zote zitahesabiwa na kubandikwa huko.”
Kwa mtazamo wa Jaji Lubuva, matokeo hayo yakibandikwa vituoni, kila mtu atajua diwani kapata kura ngapi, mbunge na hata rais aliyemchagua. Itakuwa tofauti na zamani ambapo kura zilikuwa zinasafirishwa na kuhesabiwa wilayani ambako watu wengine walidhani matokeo halisi yanabadilishwa.
Uamuzi huu tunaona ulikuwa wa lazima, ingawa umechelewa kuchukuliwa kwa kuwa malalamiko dhidi ya matokeo ya uchaguzi ni ya muda mrefu, na hakukuwa na juhudi zinazoonekana za kuyafanyia kazi.
Pamoja na kwamba kubandika matokeo ya urais vituoni hakuwezi kuwa kipimo pekee cha uchaguzi kuwa huru na haki, sisi tunaamini kwamba huo ni mwanzo mzuri wa kuelekea katika uwazi unaohitajika katika upigaji na kuhesabu kura.
Ni imani yetu pia kwamba Tume ya Taifa ya Uchaguzi itaendelea kufanyia kazi maeneo mengine, ambayo bado yanalalamikiwa kama kitendo cha kura kupigwa kwa mtindo wa kawaida licha ya kuwapo daftari la wapigakura la kielektroniki pamoja na usafirishaji wa kura kutoka eneo moja kwenda jingine.
Matarajio ya wengi ni kwamba Serikali iendelee kufanya mabadiliko ya msingi kwenye Tume na kuiwezesha kuendesha uchaguzi ulio huru, haki na wazi kwa viwango vinavyohitajika.
Wakati Tume inaendelea kufanya yaliyo ndani ya uwezo wake, Serikali inatakiwa iendelee kuandaa mazingira ya kisheria yatakayowezesha uchaguzi kuwa huru na haki, ili kuhakikisha matokeo ya uchaguzi yanaendana na kura zilizopigwa na hivyo kuondoa malalamiko yasiyokuwa ya msingi.
Katika mchakato wa Katiba Mpya yalikuwapo masuala yanayohusu uchaguzi na kwamba Katiba Iliyopendekezwa ilikuwa na kipengele cha Tume Huru ya Uchaguzi, endapo mchakato huo utaendelezwa, suala hilo na mengine yanayokusudia kuufanya uchaguzi kuwa wa haki na huru pia yazingatiwe
Kwa kutambua kuwa amani ni tunda la haki, tunaamini kwamba kitendo chochote cha kuchezea haki za wananchi katika masuala ya msingi, kama Uchaguzi Mkuu ni ishara ya wazi ya kucheza na amani na utulivu wa nchi.
Tunavishauri vyombo vya ulinzi na usalama kufanya kila linalowezekana, kuhakikisha wadau wote wa uchaguzi kila mmoja anatimiza wajibu wake ili kuhakikisha Taifa linabaki salama.
No comments:
Post a Comment