Zoezi la uokoaji zinaendelea katika
pwani ya Libya baada ya boti mbili zilizokuwa na zaidi ya wahamiaji 500
kuzama karibu na bandari ya Zuwara.
Watu zaidi ya ishirini na moja wameokolewa lakini mamia ya watu hawajulikani walipo wakihofiwa kufariki dunia.
Taarifa
ambazo hazijathibitishwa zinasema kuna zaidi ya miili miamoja katika
hospitali ya Zuwara, wakiwemo raia wa Syria, Bangaladesh na nchi kadhaa
za Afrika katika jangwa la Sahara.
Hadi sasa kwa mwaka huu
pekee,zaidi ya wahamiaji elfu mbili wamefariki wakijaribu kuvuka kutoka
Libya kwenda Italia kwa boti ambazo sio salama ndani ya maji.
No comments:
Post a Comment