Thursday, November 15, 2012

MWANAMKE ALISHA MTOTO KINYESI NA KUMCHOMA MOTO


MWANAMKE mmoja wa eneo la Majengo, jijini Mbeya, anadaiwa kummwagia maji ya moto, kumfungia ndani na hatimaye, kumlazimisha kula kinyesi, mtoto wa dada yake.
Akizungumza katika eneo la tukio,  Mwenyekiti wa Mtaa wa Majengo,   Habiba Mwakitabu, alisema  tukio hilo lilitokea juzi na kwamba liligunduliwa na majirani wa mwanamke huyo, baada ya kusikia sauti ya mtoto huyo akilia kwa maumivu.
Alisema baada ya kusikia kilio hicho, majirani hao walikwenda katika eneo hilo na kiini cha mtoto huyo kuteswa.
Mwakitabu alisema hata hivyo, mwanamke huyo alishindwa kutoa ushirikiano, jambo lililowalazimisha   wananchi kuanza kumshambulia kwa kipigo  .
Mwenyekiti huyo alisema baadaye, majirani walibomoa mlango wa nyumba na walipoingia ndani, walimkuta mtoto huyo akiwa uchi huku sehemu mbalimbali za mwili wake, zikiwa zinmeungua vibaya.
Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa mtaa,  upande mkono wa kushoto wa mwili wa mtoto huyo, ndiyo uliokuwa umeathirika zaidi.
Mwakitabu alisema katika mahojiano naye, mtoto huyo, alidai kuwa majeraha hayo yalitokana na mama yake mdogo kumfunga mikononi na kisha kumwagia maji ya moto na baadaye, kumlazimisha kula kinyesi chake hali.
Kwa mujibu wa mwenyekiti, maelezo hayo yaliwafanya wananchi kupandwa na jazba kiasi cha kuta kumshambulia tena mama huyo.  
Habari za awali zilisema, mtuhumiwa amekuwa akimfanya mtoto huyo ukatili wa mara kwa mara, licha ya jitihada za kumtaka aache kufanya hivyo.
Diwani wa Kata  ya Majengo,  Samuel Mamboma, aliwasili katika eneo hilo na kumbnusuru mama huyo kwa kumpeleka polisi akiwa na mtoto huyo ambaye baadaye alipelekwa hospitalini kwa matibabu.

No comments:

Post a Comment