Wananchi wa kijiji cha Ugabwa wilayani Makete wamesema zao
la pareto limekuwa msaada mkubwa kwao mara baada ya serikali kuwapatia mbegu za
zao hilo na wao
kukubali kulilima
Wakizungumza na waandishi wa habari kijijini hapo wananchi
hao wamesema zao hilo
lilianza kulimwa na kusimamiwa na kikundi kilichoundwa miaka miwili iliyopita
ambapo kwa sasa kila mwanakikundi analima katika mashamba yake
Wamesema kutokana na zao hilo kuwa na bei kubwa sokoni ya sh.2,200/=
kwa kilo moja, hawana budi kuendelea kulima pareto kwa kuwa wanaona faida yake
Kwa upande wake mhasibu wa kikundi cha pareto kijijini hapo
Bw. Alpha Mahenge amesema zao hilo
linawasaidia kujikwamua na changamoto mbalimbali ikiwemo kuwatimizia mahitaji
watoto wao ambao ni wanafunzi pamoja na kutunza familia
Katika hatua nyingine katibu wa kikundi hicho Bw. Ezekiel
Mahenge amesema serikali imewapa mbegu kwa ajili ya kuotesha na miche hiyo
wataigawa kwa wanakikundi ili wakaioteshe kwenye mashamba yao
Naye mwenyekiti wa kijiji hicho Bi. Rose Chaula ameishukuru
serikali kwa kutambua kwa kuwahimiza wanaugabwa kulima pareto pamoja na
wananchi wa kijiji chake kukubali kulima zao hilo na kuahidi kuendelea kuwahimiza wananchi
wote kulima pareto
Na Furahisha Nundu
No comments:
Post a Comment