Tuesday, May 8, 2012

Quran Yachomwa Moto Tena Marekani



NewsImages/6382646.jpg
Mchungaji Terry Jones alipoichoma moto Quran kushinikiza mchungaji wa Iran aachiwe huru

Mchungaji wa Marekani ambaye alizua kizaazaa mwaka jana alipoichoma moto Quran na kuweka video online, amezua tena balaa jingine kwa kuichoma moto Quran safari hii akisema anapinga kutupwa jela kwa mchungaji wa kanisa moja nchini Iran.
Mchungaji wa kanisa la Florida, Terry Jones, ambaye mwezi machi mwaka jana alisababisha mtafaruku duniani alipoichoma moto Quran, amezua balaa kwa mara nyingine kwa kuichoma moto Quran na picha walizozichora wakidai ni za mtume.

Tukio la kuchomwa moto Quran lilifanyika jumamosi usiku kwenye kanisa la mchungaji huyo la Dove World Outreach Center lililopo kwenye kitongoji cha Gainesville, Florida.

Takribani watu 20 walishuhudia tukio hilo ambapo mchungaji Jones alijifanya ni hakimu akitoa hukumu dhidi ya Quran akitaka mchungaji Youcef Nadarkhani, wa nchini Iran aachiwe huru.

Mchungaji Youcef Nadarkhani amehukumiwa kunyongwa nchini Iran kwa makosa ya uhalifu na ubakaji ambapo mashirika ya kutetea haki za binadamu yamedai sababu hasa ni kubadili kwake dini kutoka uislamu na kuingia kwenye ukristo. Alihukumiwa adhabu ya kifo mwaka 2010.

Pamoja na serikali ya Marekani kumshinikiza mchungaji Jones asihatarishe maisha ya wanajeshi wa Marekani nchini Afghanistan na kwingineko duniani kwa kuichoma moto Quran kwa mara nyingine, mchungaji Jones aliendelea na zoezi lake la kuichoma moto Quran jumamosi usiku na kulionyesha LIVE kwenye internet tukio hilo.

Mchungaji Jones aliichukua misahafu aliyoizamisha kwenye mafuta ya taa na kuichoma moto. Alichukua pia picha alizodai ni za mtume Muhammad (S.A.W) na kuzichoma moto.

Muda mfupi baada ya tukio hilo, kitengo cha zimamoto cha mji wa Gainesville kilitoa taarifa ya kulifikisha mahakamani kanisa la mchungaji huyo.

Zimamoto walidai kuwa kanisa hilo litapigwa faini ya dola 271 kwa kuchoma moto vitabu na pia litatakiwa kulipa gharama za kesi hiyo mahakamani.

Watu 12 walipoteza maisha yao sehemu mbali mbali duniani wakati mchungaji Jones alipoichoma moto Quran mwaka jana.
Askari wawili wa Marekani waliuliwa kwa kupigwa risasi nchini Afghanistan na mtu aliyevaa nguo kama polisi wa Afghanistan.

Katika historia yake, mchungaji Jones aliwahi kufukuzwa na waumini wake mwenyewe kwenye kanisa alilokuwa akiliongoza alipokuwa nchi

No comments:

Post a Comment