Thursday, March 14, 2013

TUCTA LUDEWA HATUTASHIRIKI MEI MOSI MWAKA HUU HADI KIELEWEKE. DC KUAMUA MGOGORO HUO MWEZI HUU.



Na Bazil Makungu
 Ludewa

SHIRIKISHO la Vyama vya wafanyakazi wa serikali (TUCTA)wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe wamewataka waajiri wa watumishi serikalini na wale wa mashirika ya umma kutekeleza madai na stahili zao kwanza ndipo waweze kushiriki sherehe za mei mosi mwaka huu.

Wakizungumza jana katika mkutano wa shirikisho hilo viongozi na wawakilishi wa shirikisho hilo wilayani Ludewa walisema wamechoshwa na unyanyasaji wanaofanyiwa na waajiri kwa hiyo hakuna sababu ya kushiriki katika sherehe za mwaka huu kwani haina maana.

Joseph Mvanga ni katibu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi(TUCTA) wilaya ya Ludewa akifungua mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa alisema kila mwaka wamekuwa wakishiriki maadhimisho hayo na kuandika risara ndefu lakini hakuna utekelezaji ‘’’’’ waajiri wamevaa miwani ya mbao na kuziba masikio kwa pamba hawasikii kilio na madai yetu wala hawaoni taabu tunazopata.’’’’’ Alilalamika Mvanga

Mvanga aliyataja madai na kero wanazokumbana nazo kuwa ni pamoja na watumishi kutopewa haki na stahili zao wakati wa likizo,watumishi kukaa muda mrefu katika kituo kimoja, kutopandishwa madaraja, kutolipwa malimbikizo baada ya kupandishwa madaraja.

Kero zingine ni mahusiano mabaya kati ya wakuu wa idara na watumishi waliochini yao na ugumu wa mawasiliano na wilaya, kutojibiwa barua kwa wakati na wakati mwingine kutojibiwa kabisa hii ni kero inayokatisha tamaa.

Frolian Mvanginyi ni mjumbe wa kamati tendaji ya chama cha walimu (CWT) tawi la wilaya ya Ludewa kwa upande wake akaenda mbali zaidi na kusema wao wameomba kuonana na afisa elimu tangu juni mwaka jana hadi leo hawajafanikiwa.

“”” maafisa na wakuu wa idara wamekuwa wakikisema vibaya chama cha walimu utadhani wao siyo waalimu na wamekuwa wakifanya uzembe wa makusudi wa kutowashughulikia walimu madai yao ikiwemo maazimio ya vikao kutotekelezwa kwa wakati ili kufikia malengo.’’’’ Alilalamika Mvanginyi

Kuhusu watumishi kukatwa michango mbalimbali kama mwenge kutoka katika mishahara bila ridhaa yao, wajumbe viongozi wa tucta walikemea tabia hiyo na kusema huo ni udikteta na uuaji kwa sababu hata taarifa ya mapato na matumizi ya makato hayo hayatolewi.

Naye mwalimu Samweli Mputa aliitaka ofisi ya mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo kuacha kuwapa watendaji majukumu mapya bila ya kutoa semina elekezi ili kuondoa lawama linapotokea tatizo la utekelezaji hasa kuhusu fedha na uongozi.

‘’’’’’ sisi walimu wa wilaya ya Ludewa idadi yetu inazidi 300 jambo la kushangaza afisa elimu wetu ametenga siku moja tu ya ijumaa kama siku ya kushughulikia matatizo na malalamiko ya walimu siku hiyo walimu hajaa katika ofisi hiyo bila mafanikio hiyo ni kero kubwa kwetu tunaomba tuongezewe siku.’’’’’’ Akaongeza Mputta

Horace Kolimba ni afisa utumishi katika halmashauri ya wilaya ya Ludewa, akijibu baadhi ya malalamiko na hoja za mkutano huo alikiri kuwepo kwa uzembe katika maeneo kadhaa ikiwemo wakuu wa idara katika halmashauri yake kushindwa kuwafikishia taarifa na maagizo yanayotolewa kutoka ngazi ya juu lakini akaahidi kufanya mabadiliko na kutafuta mbinu mbadala za kuwasiliana na watumishi waliopo vijijini kwa kutumia maafisa tarafa na maafisa watendaji wa kata.

Hata hivyo tucta imemtaka mkurugenzi wa halmashauri hiyo kuweka wazi fedha ya oc kwa kuzibandika katika mbao za matangazo ili kuondoa kero na malalamiko. Hata hivyo viongozi hao wametaka kuonana na mkuu wa wilaya hiyo ili kueleza kilio chao.

No comments:

Post a Comment