Tuesday, March 12, 2013

MAKETE LEO


Kiongozi wa chama cha wafanyakazi waserikali za mitaa Tanzania TALGWU amewaomba wanachama wa chama hicho kupeleka taarifa za chama kila baada ya miezi mitatu


Akizungumzia suala hilo Beatrice Njawa ambaye ni katibu wa kamati ya wanawake chama cha wafanyakazi wa serikali za mitaa taifa amesema ni jambo la msingi kwa wanachama kushiriki katika vikao vinavyofanya ili kukusanya matatizo yao yaweze kushughulikiwa

Hata hivyo ameyataja mafanikio ya chama hicho tokea kuanzia kwa mwaka 1995 chama kilikuwa na wanachama elfu 4 na kufikisha wanachama elfu 75 hadi sasa  katika mikoa yote ya Tanzania

Pamoja na mafanikio hayo Bi Njawa amezitaja baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo katika utendaji wa kazi wa chama hicho kuwa ni baadhi ya wanachama kutoshiriki katika vikao vinavyokuwa vimeandaliwa na viongozi wa chama katika ngazi ya wilaya hadi ngazi ya taifa

Katika hatua nyingine m/kiti wa TALGWU wilaya ya makte Syprian Mahenge amewashukuru viongozi kutoka ngazi ya taifa kwa kutoa elimu pamoja na ajira kwa wanachama wa chama hicho

No comments:

Post a Comment