Watoto wengi
hasa wale wa shule za awali (chekechekea) na shule za msingi kote nchini zikiwa
ni zile za watu wenye vipato vikubwa michepuo ya kiingereza au wale wa shule za
sisi akina bora kumekucha wana hekima sana.
Hekima za
watoto wetu hao inajionesha hasa pale mmoja wao anaponunua hata kitumbua kimoja
na kuweza kuwagawia wenzake hata wawe kumi.
Ni kitu
kinachoonekana ni kidogo sana lakini hiki ni kitu kikubwa sana kwasababu
kinaonesha upendo na kuwa na mtazamo wa mbele kuwa kuna siku huyo aliyenunua
leo kesho atakwama hivyo akiwagawia wenzake naye watamgawia kesho na siku
zijazo.
Lakini kitu
kama hicho kwa watu wazima wa enzi hizi ni kigumu kukiona na kukifanya kutokana
na kila mtu kujijali mwenyewe.
Kwa wenzetu
wakristo wanajua mifano hii kimaandiko hasa ukisoma katika Biblia kitabu cha 1
Wakorintho 10;23-24 ambako inasema kuwa ‘’Vitu vyote ni halali;bali si vitu
vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali bali si vitu vyote vijengavyo. Mtu
asitafute faida yake mwenyewe, bali ya
mwenzake’’ mwisho wa kunukuu.
Kwa watoto
hao hao, ukiwaambia wajisaidie kwenye sufuria ambayo anajua kuwa inatumika
kusongea ugali hawezi kukubali lakini watu wazima wa enzi hizi wapo tayari
kufanya hivyo mradi tu aliyewaambia ni mwanasiasa ambaye hata yeye hafanyi.
Hata
ukimuuliza kwanini imekuwa hivyo au
amefanya hivyo si jambo lahisi kukiri na kutubu bali atakachokifanya ni
kujitetea huku akisahau kuwa dawa ya dhambi siyo kujitetea bali ni kutubu.
Ndivyo
ilivyo hivi sasa hasa kwa watu wazima wa enzi hizi ambao wanajificha kwenye
kivuli cha kuwa wao ni wanaharakati huku wakitumia vibaya uhuru wa siasa uliopo
kwa nguzo ya kuimarisha demokrasia.
Nikiwa
safarini kuelekea mkoani Mara tarehe 19.02.2013 nilikuta pale Jijini Mwanza kuna
msongamano wa watu jioni hasa eneo la Ghana huku vijana wengine wakiwa wamevua
mashati huku jasho likiwatoka.
Kwa macho
niliona baadhi wamevaa sare za Chama cha demokrasia na Maendeleo (Chadema) na
baadhi wakawa wamevaa nguo zenye rangi anazopendelea kuvaa mwenyekiti wa chama
hicho Freeman Mbowe zile zenye rango ya kaki.
Nilipofuatilia
kuwa ilikuwaje nikaambiwa kuwa walitoka kwenye mkutano aliohutubia Mbowe siku
hiyo hivyo walikuwa wakirudi makwao kwa maandamano ambapo kila mmoja
atakapochoka anachomoka kwenye maandamano hayo ambayo nilielezwa kuwa hayakuwa
rasmi bali ulikuwa ni mzuka wa ushabiki…
Nilijaribu
kudodosa zaidi na baadaye majira ya saa mbili za usiku nikaona taarifa ya
habari iliyoonesha mkutano huo na kwamba Mbowe alitoa siku 14 kwa Waziri wa
Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dr. Shukuru Kawambwa awe amejiuzulu.
Mbowe
aliyasema hayo kwa uchungu sana akisema kuwa anatoa tamko hilo kutokana na
kufeli wanafunzi wa kidato cha Nne 2012 huku akishindwa kutoa suluhu ya tatizo
husika.
Wakati
zimebaki siku tatu kutimia siku 14 alionekana tena kwenye Luninga na vyombo
mbalimbali vya habari hapa nchini akinukuliwa kuwa sasa yeye na wenzake
wataandamana nchi nzima.
Hapo alikuwa
mkoani Mbeya ambapo sihitaji zadi kuzungumzi safari yake ilivyokuwa kwasababu sihitaji
kumfananisha na mtu anayekula matapishi yake.
Lakini ngoja
nigusie kidogo kuwa alisafiri kutoka Jijini Dar es Salaam na ndege na kutua
katika uwanja wa ndege wa Songwe uliopo nje kidogo ya Jiji la Mbeya huku gari
lake likitumia mafuta ya walipa kodi kutoka Dar es Salaam na dereva wake.
Hivyo hivyo
baada ya mkutano wake alirudi kwa ndege huku gari hilo tena la Serikali
likirejea Dar es Salaam na dereva na mafuta yakiedelea kutumika.
Swali
linabaki kuwa je ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka na fedha za umma
wanaoupinga viongozi wa Chadema na hata CCM tofauti yake ni ipi? Hapa binafsi
ni kwamba naungana mkono na wale wanaosema kuwa waliopo madarakani hatuwataki
lakini wanaotaka kuja hatuwaamini kabisa.
Katika
mkutano huo aliwachangisha wafusi wa chama hicho zaidi ya Shilingi Milioni tatu
kwa madai kuwa fedha hizo zitatumika katika kununua maji ya kunawa ili
kupambana na polisi katika maandamano yaliyotarajiwa kufanyika.
Usihoji kuwa
fedha hizo zipo wapi au akaunti ipi kwa manufaa ya nani. Kwani tulio wengi
hatuamini kuwa ndani ya Chadema kuna mafisadi na mtapeli wanaotumia njia za
kisayansi kama vilivyo vyama vingine na hata CCM inayoshutumiwa kwa kila aina
ya ‘’uchafu’’.
Hao ndiyo
watu wazima wa enzi hizi ambao hawawezi kuhoji wala kuwaza mema badala ya
mabaya huku wakitanguliza ubinafsi badala ya maslahi ya taifa.
Hawajaweza
kuhoji kuwa kwanini tununue maji ya kunawa kuzuia mabomu na kupambana na polisi
badala ya kuomba kibali cha maandamano na kutoa kero zao, hawawezi kuhoji kuwa
kwanini maandamano yasianzie Moshi safari hii badala ya Mwanza, Mbeya na
Arusha!
Wanashindwa
kufanya hivyo kwasababu wengi wamezoea kufikiriwa badala ya wao kufikiri na
kujega mashaka, hao ndiyo watu wazima wa enzi hizi.
Nampongeza
sana bosi wangu Freeman Mbowe kwa kuendelea kuangalia uelewa wa watu
anaowaongoza na hata kufikia hatua ya kuwaambia ukweli kuhusu uelewa wao mdogo
wa kiutawala ndani ya vikao vya ndani na kuwaeleza kuwa hawawezi kutawala nchi
wala kushika dola kwa siasa za harakati.
Hayo
aliyaeleza akiwa katika kikao cha ndani ukumbi wa mikutano wa Mkapa uliopo
Jijini Mbeya kabla ya mkutano wa hdhara aliowachangisha mamilioni wenye tamaa
ya kuandamana bila kujua kuwa matokeo yake ni nini wakiandamana au
wasipoandamana.
Sidhani kama
kuna RPC wa mkoa wowote atakayekubali kuulizwa na Mungu siku ya mwisho kuwa
alipokuwa kamanda wa Polisi katika mkoa huo alifanyaje kuruhusu maandamano ya
watu waliotoka katika mikoa ya jirani na kuharibu mali na uporaji wa kijinga
huku yeye akiangalia bila kuwajibika katika hilo hakika naye tutamwekea
maandamano ya kujiuzulu.
Sishawishi kuwa
wakuu hao wa polisi wazuie maandamano yenye hoja lakini katika maandamano haya
ambayo watu wanajiandaa kufanya fujo na tayari wametamka hadharani kuwa siku
hiyo wamejipanga kupambana na polisi, hapana tuwe wakweli na hapa tuwe kama
watoto wadogo si kama watu wazima wa enzi hizi.
Hebu kwa
pamoja tujiuluze kuwa, bahati mbaya yakatokea machafuko hapa nchini nani
atakayeweza hata kushauri au kutuliza ghasia kwa kuheshimika na jamii? Je
sampuli za watu wazima wa enzi hizi wanaweza? Tutafakari na tuseme imetosha
kuburuzwa bali tufikiri kwanza hata kama wao watasema…

No comments:
Post a Comment