Maelfu ya raia wa Ugirik usiku wa
leo wametawanyika katika mitaa ya mjini Anthens karibu na jengo la
bunge, wakifurahia kura ya hapana waliyoipiga ambayo imeshinda kwa ya
asilimia 60.
Waziri mkuu wa Ugiriki Alexis Tsipras,amesema matokeo
hayo ya hapana, hayana nia ya kwenda kinyume na jumuiya ya Ulaya bali
yataiongezea Ugiriki uwezo wa majadiliano zaidi kuhusiana na mzozo wa
madeni.
Tsipras ameongeza kuwa serikali ya Ugiriki iliitisha kura
hiyo ya maoni ikiamini kuwa kura ya Hapana italeta makubaliano mazuri,
pamoja na kwamba kuna onyo kutoka kwa viongozi wa ukanda wa Euro kuwa
hatua hiyo itasababisha Ugiriki kuondolewa katika nchi wananchama wa
ukanda huo.
Naye Rais wa Bunge la Jumuiya ya Ulaya Martin Schulz
amesema kuwa kura hiyo ya HAPANA inaiacha Ugiriki katika mazingira
mabaya zaidi kuhusiana na mzozo wa madeni na vikwazo vya kimataifa.
Waziri
wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier anasema kwa
matokeo hayo sasa umamuzi ni wa mahakama ya Ugiriki kwani wapiga kura
wamepinga kwa nguvu zote masharti ya wakopeshaji wa kimataifa
Matokeo
haya yanasababisha kukubalika zaidi kwa Waziri mkuu wa Ugirik Alexis
Tsipras japo kuwa pia anakuwa na wajibu mkubwa wa kukabiliana na
mazingira yote ya kipindi hiki cha mpito kuhusiana na mzozo wa madeni.
No comments:
Post a Comment