Sunday, June 14, 2015

MZEE YUSUPHU ATANGAZA NIA RASIMI

MZEE YUSUF AANGUSHA BONGE LA BURDANI, ATANGAZA NIA DAR LIVE

...Akitangaza nia ya kugombea ubunge.
Mzee Yusuf akiwaonesha mashabiki wake tuzo za Kili alizozoa usiku huo.
...Akiwaangushia mashabiki wake burudani
.
Nyomi ya watu wakiserebuka.
Baadhi ya waimbaji wa bendi hiyo wakiwa katika pozi mwanana.
Mwimbaji wa Jahazi Modern Taarab, Prince Amigo, akitumbuiza.
KAMA kawaida yake, mfalme wa muziki wa mwambao, Mzee Yusuf,  na kundi lake la Jahazi Modern Taarab, usiku wa jana aliangusha bonge la burudani kwa mashabiki katika Ukumbi wa Taifa wa Burudani wa Dar Live ulioko Mbagala-Zakhem jijini Dar es Salaam.
Burudani hiyo ilifanyika sambamba na kutambulishwa kwa nyimbo zao mpya katika albamu ya ‘Mahaba Niue’ na kutangaza kwamba atagombea ubunge mwaka huu katika jimbo moja huko Mjini Magharibi, Zanzibar, katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment