Saturday, June 13, 2015

ANGALIA MPAMBANO WA DIAMOD NA ALIKIBA


Ni nani kama Msuva? Jina hilo, Simon Happygod Msuva si geni katika medani ya michezo nchini.
Juzi, aligeuka habari ya mjini baada ya kutwaa tuzo mbili katika hafla maalumu iliyoandaliwa na wadhamini wakuu wa Ligi Kuu, Kampuni ya Simu za Mkononi, Vodacom.
Tuzo hizo ni ile ya mfungaji bora wa msimu wa 2014/15 sanjari na ile ya mchezaji Bora wa msimu huo uliomalizika mwezi uliopita na timu yake, Yanga kutwaa ubingwa. Kwa kutwaa tuzo hizo, mshambuliaji huyo wa Yanga na Taifa Stars aliweka kibindoni zaidi ya Sh11 milioni.

Kivutio kikubwa kwenye hafla hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Golden Jubilee, Posta Mpya jijini Dar es Salaam, ilikuwa ni familia ya Msuva iliyomwakilisha mchezaji huyo aliyeko Misri kwenye kikosi cha Stars kinachoikabili Misri kesho kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Afrika 2017.
Wazazi wake, Happygod na Suzane ambao walipokea tuzo hiyo hawakuficha furaha yao wakati wa hafla hiyo.
Hata hivyo, alikuwa baba, Mzee Happygod ambaye alitumia muda huo kueleza mengi kuhusu mwanaye huyo na mapenzi yake makubwa katika soka.
Alisema kipaji cha mwanaye huyo mwenye umri wa miaka 23, kilianzia Shule ya Msingi Lions iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam, lakini kiliendelea alipokuwa Shule ya Sekondari ya Midland iliyoko pia Dar es Salaam.
Atamba ‘Uhai Cup’, Azam, Simba
zampotezea.
Baada ya kucheza soka la mtaani kwenye timu ya Wakati Ujao, ambayo hufanya mazoezi yake kwenye viwanja vya Chuo Kikuu Dar es Salaam na kufanya vizuri, 2009 aliteuliwa katika timu ya Kinondoni iliyoshiriki mashindano ya Copa Coca Cola alikoshika nafasi ya pili kwa ufungaji.
Kutokana na kufanya kwake vizuri, Azam ilimchukua katika timu yao ya vijana aliyoichezea kwenye mashindano ya Kombe la Uhai 2010, ambako aliibuka mfungaji bora.
Hata hivyo, Msuva hakupata mkataba wa kuchezea kikosi cha wakubwa cha Azam, ndipo akaangukia mikononi mwa Moro United kabla ya kusajiliwa rasmi na Yanga anayoichezea hadi sasa.

No comments:

Post a Comment