Monday, May 25, 2015

KABURI LENYE MIILI ZAIDI YA 100 ALAONEKANA MALAYISIA

Malaysian national police chief Khalid Abu Bakar speaks during a press conference a day after the government announced the discovery of camps and graves, the first such sites found in Malaysia since a regional human-trafficking crisis erupted earlier this month, near Malaysia-Thailand borders in Wang Kelian on May 25, 2015.
 

Makaburi yasiyopungua 30 yanayosadikiwa kuwa na viwiliwili vya wahamiaji kutoka Myanmar na Bangladesh yamegunduliwa katika jimbo la kaskazini mwa Malaysia la Perlis. Kwa mujibu wa gazeti la Star, miili ipatayo 100 ilipatikana kwenye kaburi moja la umati siku ya Ijumaa. Waziri wa Mambo ya Ndani wa Malaysia Zahid Hamidi amesema makaburi hayo yamepatikana kwenye kambi 17 zilizohamwa za kuhifadhi watu wanaosafirishwa kwa njia ya magendo. Makaburi kadhaa ya umati yamegunduliwa nchini Thailand katika njia inayotumiwa na Waislamu wa Rohingya wanaokimbia mateso nchini Myanmar. Lakini hii ni mara ya kwanza kwa makaburi kama hayo kugunduliwa nchini Malaysia. Wakati huohuo Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch limekosoa vikali sheria mpya ya idadi ya watu iliyosainiwa na Rais wa Myanmar Thein Sein likisema, sheria hiyo inailenga jamii ya wachache ya Waislamu wa kabila la Rohingya. Sheria hiyo iliyosainiwa tarehe 19 mwezi huu, pamoja na mambo mengine inaruhusu serikali za majimbo kuanzisha mpango wa uzazi wa mpangilio ili kupunguza ongezeko la kizazi. Serikali ya Myanmar haiwatambui Waislamu wa Rohingya kuwa ni raia wa nchi hiyo, ikisisitiza kuwa ni wahamiaji haramu licha ya kuishi nchini humo kwa karne kadhaa…/

No comments:

Post a Comment