RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AONGOZA MAZISHI YA BI KIDUDE
Licha
ya mvua kubwa iliyonyesha katika maeneo ya kijiji cha Kitumba Wilaya ya
Kati, Mkoa wa kusini, Unguja, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ,
Dk. Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Sheni
leo mchana waliwaongoza maelfu ya Watanzania na wasanii mbali mbali
katika maziko ya msanii mkongwe nchini Tanzania Fatma Bint Baraka Khamis
‘Bi. Kidude’.
Maziko
hayo yaliyotanguliwa na sala maalum iliyofanyika baada ya swala ya
adhuhuri katika msikiti wa Mwembeshauri, mjini Zanzibar ambayo
ilihudhuriwa pia na makamo wa Rais wa Tanzania Dk. Mohammed Gharib
Bilal na Makamo wawili wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na
Balozi Seif Ali Iddi na viongozi wengine kadhaa wa serikali na taasisi
za sanaa nchini.
Aidha wasanii mbali mbali wakiwemo wa taarab na muziki wa kizazi kipya wa ndani na nje ya Zanzibar walihudhuria katika mazishi hayo yaliyoongozwa na Kadhi Mkuu wa Zanzibar , Sheikh Khamis Haji.
Mwili
wa marehemu Bi Kidude uliokuwa umepakiwa katika gari maalum la polisi
lenye namba PT 1891 uliongoza msafara kuelekea katika makaazi ya milele
ya msanii huyo maarufu majira ya saa 7.10 mchana na kufika katika eneo
la makaburi ya familia ya marehemu huyo majira ya saa 7.32 na taratibu
za mazishi kusita kwa muda ili kupisha mvua kubwa iliyoanza kunyesha
muda mchache baada ya msafara huo kufika katika maeneo ya Mwera kilomita
chache kabla ya kufika eneo la mazishi.
Mbali
na mvua hiyo kunyesha kwa wingi kijijini hapo bado maeneo mengi ya
Zanzibar ikiwemo mjini yalikuwa makavu jambo lililotafsiriwa kuwa ni
baraka hasa ikizingatiwa kuwa hakukuwa na mvua iliyonyesha kijijini hapo
na katika maeneo ya karibu kwa zaidi ya siku tatu.
Akisoma
risala kwa niaba ya serikali ya Zanzibar, mkuu wa utangazaji wa shirika
la utangazaji Zanzibar, ZBC, Hassan Vuai alisema serikali inatambua
mchanago wa marehemu katika kukuza sanaa ndani na nje ya nchi na kwamba
inamtambua na kumuweka katika orodha ya watu maarufu wenye mchango kwa
Zanzibar.
“Serikali
ya Zanzibar inatambua mchango wa marehemu na itazikusanya kazi zake na
kumbukumbu nyengine na kuziweka katika makumbusho ya taifa ili lwe
urithi kwa vizazi vijavyo”, alisema Vuai.
Aliongeza
kuwa hali hiyo haitokani na umahiri wa marehemu katika kukuza sana ya
muziki wa asiia bali pia umuhimu wake kwa jamii kutokana na kuwa ni
miongoni mwa matabibu wa dawa asilia aliekuwa akisafiriwa sana na jamii
ya watu wa Zanzibar.
Akizungumza
na waadshi Rais Kikwete alisema licha ya kuupokea taarifa za msiba huo
kwa mshtuko alisema msiba huo ni pigo kubwa kwa wasanii wachanga ambao
katika siku za karibuni walikuwa wakimshirikisha katika kazi zao.
“Hili
si pigo kwa nchi pekee bali wasanii wachanga kwani bado naamini
walikuwa wakimuhitaji kufanya nae kazi na kuchota ujuzi wake”, alisema
Kikwete.
Awali
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alitoa ubani wa shilingi
Milioni 2,000,000/- kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa
familia ya marehemu na kuwataka kuelewa kuwa jamii
na waswahili wa mwambao wa Afrika Mashariki wanafahamu mchango msanii
katika fani ya muziki wa taarabu na kwamba hawatasita kuuenzi.
Alisema
Zanzibar imepata sifa kubwa katika nyanja za Kimataifa kutokana na
mchango wa wasanii wake kueneza sanaa ya taarabu iliyotoa fursa kwa
baadhi ya watalii na wataalamu wa sana kuitembelea Zanzibar kwa lengo la
kufanya utafiti au hata kushuhudia umahiri wa wasanii waliopo akiwemo
Bi. Kidude.
Makamu
huyo wa Rais wa Zanzibar aliitaka Familia ya ‘Bi Kidude’ kuwa na moyo
wa subra katika kipindi hichi kigumu cha msiba na kuwaeleza kwamba msiba
huo sio wao peke yao .
“
Kwa kweli sisi sote tunampenda sana Bi Fatma Binti Baraka ‘Bi Kidude’
lakini tuelewe kwamba Mwenyezi Mungu anampenda zaidi na ndio maana
akamuhitaji”. Alinasihi Balozi Seif.
Naye
Mmoja wa wana Familia hiyo Bwana Haji Ramadhan Suwed Buda kwa niaba ya
Familia ya Marehemu Bi Kidude ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar kwa mchango wake wa kuungana nao katika msiba huo.
Bwana Haji alisema hatua hiyo ya Serikali imeleta faraja kwao na kupunguza machungu ya msiba huo.
Msanii
Gwiji wa sanaa ya Taarab asilia na ngoma ya Unyago, Bi Kidude
aliyekadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 98 hakuwahi kuzaa mtoto
licha ya kuolewa mara mbili katika uhai wake.
Mwenyezi Muungu ailaze roho ya marehemu 'Bi Kidude' mahali pema peponi amin.
No comments:
Post a Comment