Saturday, February 9, 2013

MAKINDA AFUTA KAMATI YA ZITOO

 
Zitto Kabwe 

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda ametangaza mabadiliko ya Kamati za Kudumu za Bunge, huku Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) iliyokuwa ikiongozwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ikifutwa.
Kutokana na mabadiliko hayo, shughuli za POAC sasa zitaendelea kufanywa na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), ambayo itaendelea na jukumu lake la msingi la kuchambua taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na kwa Serikaki Kuu.

Kamati nyingine iliyofutwa ni ya sheria ndogo, huku Spika akiunda kamati mpya tatu na nyingine kuzifanyia marekebisho kadhaa ikiwa ni hatua ya kuimarisha usimamizi wa Bunge kwa shughuli za Serikali. 


No comments:

Post a Comment