Saturday, February 16, 2013

ANGALIA VURUGU ZA POLISI NA WAISILAMU DAR


8Wafuasi hao wa Shekh Ponda wakipandishwa kwenye gari la polisi mara baada ya kukamatwa katika maandamano hayo.

 Licha ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam kuzuia maandamano ya Waumini wa Dini ya Kiislam, baadhi ya watu wanaodaiwa kuwa ni Waumini wa Dini hiyo katika maeneo ya Buguruni, Malapa na Kariakoo wamefanya maandamano hayo.
Hata hivyo Jeshi la Polisi kupitia Vikosi vya Kutulia Ghasia-FFU-limelazimika kutumia Mabomu ya Machozi ili kuwatawanya waandamanaji hao waliokuwa wamebeba Mabango na Mawe kwenye Mifuko katika Mitaa ya Malapa pamoja na Kariakoo.
mtandao  huu  wa www.francisgodwin.blogspot.com umeshuhudia Maduka mbalimbali yakiwa yamefungwa katika Mitaa ya Kariakoo kutokana na maandamano hayo ya watu wanaodaiwa kuwa Waumini wa Dini ya Kiislam.
Waumini hao wanashinikiza Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa Mashitaka-DPP-kumwachia kwa dhamana Katibu wa Jumuiya ya Waislam Shekh PONDA ISA PONDA ambaye anakabiliwa na kesi ya uchochezi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Jana Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar e s salaam kupitia kwa Kaimu Kamanda wake AHMED MSANGI lilipiga marufuku kufanyika kwa mandamano hayo kutokana na kutokuwa na kibali cha Polisi.
 
 

FFU WATUMIA MABOMU YA MACHOZI KUTAWANYA WAISLAMU ENEO LA KARIAKOO LEO


3Poalisi wakiimarisha Doria katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.
Hapa  sio maduka  yamefungwa  muda  umepita ama  wahusika  wamefiwa hapana ni baada ya vurugu  kutokea
Hii ni kariakoo sio biashara  mbaya ni usalama hakuna
6 Askari Polisi wakifanya doria kwa kutumia pikipiki kam wanavyoonekana wakiranda katika mitaa mbalimbali Posta jijini Dar es salaam.
7 Baadhi ya wafuasi wa Shekh Ponda wakiwa wamekamatwa kwa tuhuma za kufanya maadamano bila kibali cha polisi.
8Wafuasi hao wa Shekh Ponda wakipandishwa kwenye gari la polisi mara baada ya kukamatwa katika maandamano hayo.
9 Zoezi la kuwakamata na kuwapeleka polisi watuhumiwa hao likiendelea chini ya ulinzi mkali.
10Magari mbalimbali yakiwa yamebeba askari Polisi yakipita mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.
11 
Polisi wa Pikipiki wakiwa kazini leo.
Habari  kutoka  jijini Dar es Salaam  zinadai kuwa  jeshi la  polisi jijini hapo  limelazimika  kutumia mabomu ya machozi  kuwatawanya  baadhi ya  wafuasi wa dini ya kiislam ambao  walikuwa  wakiandamana  eneo la Kariakoo  kama njia ya kushinikiza  kuwachiwa huru kwa Shekh Ponda.
Mwandishi  wa mtandao  huu  wa www.francisgodwin.blogspot.com kutoka jijini Dar es Salaam Calros  Mtoye anaripoti kuwa hali  hiyo imejitokeza mchana  wa leo na kuwa  kutokana na  polisi  kutumia mabomu hayo ya machozi  wafanyabiashara  wa eneo hilo la Kariakoo  wamelazimika kuyafunga maduka yao kwa muda.
 

No comments:

Post a Comment