Thursday, November 15, 2012

ZAIDI SHILINGI MILONI MBILI ZATUMIKA KATIKA UKARABATI WA MAJENGO KISINGA MAKETE



Zaidi ya shilingi milioni mbili na laki nne zimetumika katika ukarabati wa baadhi ya majengo katika shule ya msingi Kisinga kata ya Lupalilo wilayani Makete

Akizungumza ofisini kwake mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kisinga Bi. Tulumbe Kyando amesema kuwa ukarabati wa shule hiyo ni pamoja na vyoo vya nyumba za waalimu, madarasa saba na ofisi mbili za waalimu

Amesema wakati wa ukarabati huo wananchi nao walikuwa wakishiriki zoezi hilo ambalo lilikuwa likifanyika siku za mwisho wa wiki Ijumaa na Jumapili

Mwalimu Kyando amesema fedha hizo zilizotumika kwa ajili ya ukarabati hazikuchangwa na wananchi kama ilivyozoeleka badala yake zimetokana na kuuzwa sehemu ya msitu wa shule hiyo, ambapo fedha hizo zimetumika kununua saruji, mchanga, mbao pamoja na vioo

Mwalimu huyo amemshukuru afisa mtendaji wa kijiji hicho pamoja na wananchi kwa kutoa ushirikiano kufanikisha ukarabati huo, kwani hiyo ni njia mojawapo ya kuboresha elimu wilayani Makete

Katika hatua nyingine Afisa mtendaji wa kijiji cha Kisinga Bw. Raphael Tweve amesema katika ukarabati huo waliweka mkakati wa kusogeza maji shuleni hapo, mkakati ambao wameutekeleza

Amesema hapo awali kulikuwa na tatizo la shule hiyo kukosa maji, lakini kwa hivi sasa tatizo hilo litatoweka

No comments:

Post a Comment