>>AVB akata tamaa Ubingwa, ataka nafasi ya 4 tu!!
>>AKIRI BINGWA Ni Man United, City au Chelsea, walobaki kugombea 4!
Ili
kuishika nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu England ili wapate fursa ya
kucheza Ulaya kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI, Andre Villas-Boas anaamini
Tottenham ni lazima wamalize Ligi wakiwa juu ya Arsenal Msimu huu.
Lakini mara ya mwisho kwa Tottenham
kumaliza Ligi wakiwa mbele ya Arsenal ni Mwaka 1995 wakati hata Arsene
Wenger, Meneja wa sasa wa Arsenal, hajaanza kibarua.
Msimamo huo wa Villas-Boas umetolewa
kwenye mahojiano na Wanahabari kuhusu Dabi yao na Arsenal itakayochezwa
Jumamosi Uwanja wa Emirates.
Villas-Boas alijibu swali kuhusu nini
lengo lao Msimu huu kwa kusema: “Ninachoona ni dhahiri Man United, Man
City na Chelsea wapo kwenye mbio kubwa za Ubingwa. Ingawa ngumu kumaliza
nafasi ya 4 lakini ni lazima tumalize juu ya Arsenal ili kuipata.”
++++++++++++++++++++++++
DONDO za DABI: Arsenal v Tottenham
-Tottenham wamepoteza Mechi moja tu kati ya 5 walizocheza mwisho na Arsenal.
-Magoli 100 yamefungwa katika Dabi 32 tangu Arsene Wenger atue Arsenal
++++++++++++++++++++++++
Kimsimamo, kwa sasa, Tottenham wapo nafasi ya 7 wakiwa Pointi 1 mbele ya Arsenal walio nafasi ya 8.
Tottenham wapo Pointi 7 nyuma ya Timu ya 3 Chelsea na Pointi 10 nyuma ya vinara Manchester United.
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO Timu za juu:
1 Man United Mechi 11 Pointi 27
2 Man City Mechi 11 Pointi 25
3 Chelsea Mechi 11 Pointi 24
4 Everton Mechi 11 Pointi 20
5 WBA Mechi 11 Pointi 20
6 West Ham Mechi 11 Pointi 18
7 Tottenham Mechi 11 17
8 Arsenal Mechi 11 Pointi 16
+++++++++++++++++++++++
Msimu uliopita Arsenal walimaliza wakiwa
nafasi ya 3 na Tottenham nafasi ya 4 lakini Tottenham hawakupewa nafasi
ya kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI kama ilivyotakiwa kwa vile Chelsea
walitwaa Ubingwa wa UEFA CHAMPIONZ LIGI na hivyo kupewa nafasi ya
kutetea Taji lao na Tottenham kutupwa kwenye EUROPA LIGI.
Wakati huo huo, Villas Boas
amethibitisha Kiungo wa Belgium Mousa Dembele hatacheza Dabi hiyo na
Arsenal kwa vila bado ana tatizo la nyonga.
Baada ya kuumia nyonga, Dembele amezikosa Mechi 8 za Tottenham.
+++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi, Novemba 17, 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Arsenal v Tottenham Hotspur
[SAA 12 Jioni]
Liverpool v Wigan Athletic
Manchester City v Aston Villa
Newcastle United v Swansea City
Queens Park Rangers v Southampton
Reading v Everton
West Bromwich Albion v Chelsea
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Norwich City v Manchester United
Jumapili, Novemba 18, 2012
[SAA 1 Usiku]
Fulham v Sunderland
Jumatatu, Novemba 19, 2012
[SAA 5 Usiku]
WestHam v Stoke City
MAREFA-Ratiba ya Mechi zao:
Jumamosi Novemba 17
Arsenal v Tottenham
Refa: H Webb
Refa Wasaidizi: M Mullarkey, D Cann
Refa wa Akiba: C Foy
Reading v Everton
Refa: M Atkinson
Refa Wasaidizi: P Kirkup, J Flynn
Refa wa Akiba: A Marriner
West Bromwich Albion v Chelsea
Refa: M Oliver
Refa Wasaidizi: S Child, D England
Refa wa Akiba: S Attwell
Manchester City v Aston Villa
Refa: J Moss
Refa Wasaidizi: S Beck, A Holmes
Refa wa Akiba: L Probert
Newcastle United v Swansea City
Refa: P Dowd
Refa Wasaidizi: A Garratt, S Ledger
Refa wa Akiba: A Bates
Queens Park Rangers v Southampton
Refa: M Dean
Refa Wasaidizi: J Collin, J Brooks
Refa wa Akiba: L Mason
Liverpool v Wigan Athletic
Refa: K Friend
Refa Wasaidizi: R Ganfield, A Halliday
Refa wa Akiba: J Adcock
Norwich City v Manchester United
Refa: A Taylor
Refa Wasaidizi: R West, P Bankes
Refa wa Akiba: N Swarbrick
Jumapili Novemba 18
Fulham v Sunderland
Refa: L Probert
Refa Wasaidizi: D Bryan, L Betts
Refa wa Akiba: A Marriner
Jumatatu Novemba 19
West Ham United v Stoke City
Refa: C Foy
Refa Wasaidizi: H Lennard, M McDonough
Refa wa Akiba: H Webb
No comments:
Post a Comment