Hawa ndo nyani wanao haribu mazao huko Utanzawa
Na Hadija Sanga
Kumeibuka wimbi
la wanyama waharibifu katika kijiji cha Utanziwa kata ya Bulongwa
wilayani Makete ambao wanaharibu mazao yaliyopo mashambani pamoja na
mifugo ya wakazi hao
Akizungumza na
wandishi wetu ofisini kwake, afisa mtendaji wa kijiji hicho Bw. Paulo
Simon Chaula amesema kuwa kijiji hicho kinakabiliwa na wanyama
waharibifu wa mazao ambapo kwa kiasi kikubwa wamesababisha hasara kwa
wakazi hao
Amesema wanyama
hao waharibifu wa mazao ni jamii ya nyani ambao wameanza uharibifu huo
bila ya wao kujua walipotokea ambapo mpaka sasa bado wanaendelea na
uharibifu huo
Amesema wao kama kijiji kinawataka wakazi hao kuwafukuza wanyama hao wakati wanafanya utaratibu wa kulifikisha suala hilo kwenye ngazi husika kwa kuwa sheria haziruhusu kuwaua wanyama hao
Wilaya ya Makete
ni miongoni mwa wilaya yenye hifadhi ya taifa amapo inaamnika wanyama
hao waharibifu wa mazao hutokea humo na kwa mujibu wa sheria hairuhusiwi
kuwaua wanyama hao



No comments:
Post a Comment