Asasi zisizo za
kiserikali wilayani Makete zimeshauriwa kuwashirikisha wataalamu wakati
wa uanzishwaji wa miradi mbalimbali ili kupewa ushauri wa kitaalam
utakaoweshesha miradi hiyo kufanikiwa kama walivyopanga
Rai hiyo imetolewa kwenye kikao cha wadau wa shirika la MASUPHA kilichofanyika kwenye ukumbi wa shirika hilo kwa lengo la kuona ni namna gani shughuli zinazofanywa na shirika hilo zitafanikiwa zaidi
Akichangia hoja
kwenye kikao hicho afisa maendeleo ya jamii wilaya ya Makete Bw. Focus
Mwita amesema kuwa mashirika mengi yaliyoanzishwa wilayani hapo mengi
yamekufa kutokana na kuanzisha miradi ambayo whawakuwashirikisha
wataalamu hiyo malengo hayakutimia hali iliyosababisha ukomo wa
mashirika hayo
“Unakuta shirika
linaanzisha tuseme mradi wa kuku kwa wanachama wake, sasa badala ya
kumchukua Afisa mifugo na akashirikishwa kwanza kuona kama kuku hao
watafaa kwa muda huo ama vipi, na kama kuku hao watanunuliwa mbali je wataweza kuishi Makete? Hili litasaidia sana kufanikisha kwa miradi hiyo” alisema Mwita
Pia Mwita
ameshauri asasi hizo kufanya upembuzi yakinifu kuwa ni sehemu gani
mashirika mengine hayajajikita kusaidia jamii ile ili sehemu kama
hizo zipelekewe miradi hiyo ili kuepuka suala la asasi nyingi kufanya
shughuli kwenye maeneo yale yale huku mengine yakikosa miradi
Kwa upande wake
mratibu wa Ukimwi wilaya ya Makete Dkt. Shadrack Sanga amesema kuwa kwa
kuwa shirika hilo la MASUPHA limeamua kuibua mradi wa kutoa elimu ya VVU
kwa walemavu, kwa wakati mwingine lione ni namna gani ya kusaidia
mahitaji mengine ya walemavu ikiwemo fimbo kwa ajili ya walemavu
wasioona ama baiskeli kwa walemavu wa miguu
Amesema wakati
mwingine wanapofanya tathmini kwa walemavu huko vijijini wapo baadhi ya
walemavu ambao kwa namna nyingine ulemavu wao unaweza kupona endapo
watapatiwa matibabu na wataalam, hivyo ni vyema shirika hilo likaona ni namna gani ya kuwaunganisha na hospitali ya CCBRT kwa matibabu zaidi
Katika hatua
nyingine msemaji baadhi ya wanavikundi wa MASUPHA ambao walinufaika na
mradi wa mbuzi uliotolewa kwao hivi karibuni na shirika hilo
wameshauri kupatiwa elimu zaidi ya namana ya kuwatunza`mbuzi hao wa
kisasa kutoka kwa wataalamu wa mifugo ili lengo la kupatiwa mradi huo
lifikiwe kikamilifu
Mkurugenzi wa shirika hilo Bi. Aida Chengula amesema ao kama
shirika wamechukua mapendekezo waliyopatiwa na wadau hao na kuahidi
kuyafanyia kazi kwa kushirikiana na wafadhili wao huku akiwataka
wananchi wanaoletewa miradi hiyo kuhakikisha inafanikiwa licha ya
changamoto za hapa na pale
Amesema ni vigumu kutimiza mahitaji ya watu kwa mara moja lakini kwa kupitia miradi inayoendeshwa na shirika hilo itasaidia kutatua kero za wananchi hao kwa kiasi kikubwa


No comments:
Post a Comment