Wednesday, November 21, 2012

UTANZIWA WAFANYA KWELI BARABARA ZA MITAA


Ukarabati wa barabara za mitaa katika kijiji cha Utanziwa kata ya Bulongwa wilayani Makete umefanywa na wakazi wa kijiji hicho ili kujiletea maendeleo kijijini hapo baada ya kutegemea selikari pekee

Akizungumza na mwandishi wetu ofisini kwake Afisa mtendaji wa kijiji hicho Bwana Paulo Chaula amesema zoezi hilo linafanya na nguvu za wananchi wa kijiji hicho hadi kumalizika kwake

Amesema ukarabati huo ambao ni upanuzi wa barabara hizo umeanzia Zahanati ya Utanziwa hadi shuleni

Amesema ingawa wananchi hao hawakuwa na vifaa vyote vinavyohitajika wakati wa kufanya kazi hiyo lakini anashukuru kuwa zoezi hilo limefanikiwa huku akiitaka serikali kutembelea kijijini hapo kukagua shughuli za maendeleo zinazofanywa na wananchi wake

Na Hadija Sanga



No comments:

Post a Comment