Wednesday, November 21, 2012

CHELSEA YAMTIMUA DI MATTEO YA MTAKA BENTEZ








Chelsea imetangaza kumfukuza kazi Meneja wake Roberto Di Matteo mara baada ya jana kuchapwa Bao 3-0 na Juventus kwenye Mechi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI ambayo imewaweka katika hali ngumu kusonga mbele Raundi inayofuata na hivyo kuwa hatarini kulitetea Taji lao la Ubingwa wa Ulaya.
Msimu uliopita Di Matteo alitwaa UEFA CHAMPIONZ LIGI na FA CUP akiwa Meneja wa muda na Mwezi Juni alisaini Mkataba mpya wa Miaka miwili uliomsimika kama Meneja wa kudumu.
Chelsea, ikitoa taarifa ya kufukuzwa Di Matteo, pia imesema watatangaza hivi karibuni nani atashika wadhifa wa Meneja.
++++++++++++++++++++++++++++++
HIMAYA ya ROMAN ABRAMOVICH=MAMENEJA:
-Claudio Ranieri: Septemba 2000-Mei 2004
-Jose Mourinho: Juni 2004-Septemba 2007
-Avram Grant: Septemba 2007-Mei 2008
-Luiz Felipe Scolari: Julai 2008-Februari 2009
-Guus Hiddink: Februari 2009-Mei 2009
-Carlo Ancelotti: Juni 2009-Mei 2011
-Andre Villas-Boas: Juni 2011-Machi 2012
-Roberto di Matteo: Machi 2012-Novemba 2012
++++++++++++++++++++++++++++++
Inaaminika Mmiliki wa Chelsea, Tajiri Roman Abramovich, ameshafanya mazungumzo na Meneja wa zamani wa Liverpool Rafael Benรญtez ili ashike wadhifa wa Meneja.
Chelsea walianza vyema Msimu huu kwa kushinda Mechi 7 kati ya 8 za kwanza kwenye Ligi na kutwaa uongozi lakini tangu wachapwe 3-2 na Manchester United Uwanjani kwao Stamford Bridge wamezidi kudidimia na wameshinda Mechi mbili tu kati ya 8 za mwisho.
Kwa sasa wapo nafasi ya 3 kwenye Ligi Kuu England wakiwa Pointi 4 nyuma ya vinara Manchester City ambao Jumapili ijayo watapambana nao Uwanjani Stamford Bridge kwenye Mechi ya Ligi.
Ikiwa Chelsea watashindwa kuvuka hatua ya Makundi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, kitu ambacho ni kigumu hasa kwa vile kwenye Kundi lao Shakhtar Donetsk washafuzu na Juventus wanahitaji sare watakapocheza na Shakhtar katika Mechi ya mwisho ili wafuzu, itawafanya Chelsea waweke historia ya kuwa Mabingwa wa kwanza watetezi kushindwa kuvuka hatua ya Makundi.
Hivi sasa, Abramovich anasaka Meneja wake wa 9 tangu yeye mwenyewe atue Stamford Bridge Mwaka 2003.

No comments:

Post a Comment