Monday, November 12, 2012

WAANDISHI WA HABARI WAMETAKIWA KUANDIKA HABARI ZA KICHUNGUZI ILI KUIBUA MAMBO YALIYOJIFICHA



KATIBU WA chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa IPC bwana Frank Leonard akitoa mafunzo ya siku mbili kwa wanahabari wa kituo cha Radio Uplands fm.
Wanahabari wa kituo cha UPLANDS FM RADIO NJOMBE WAKIWA KATIKA MAFUNZO

Waandishi wa Habari Wametakiwa Kuandika Habari ya Uchunguzi Zaidi Ili Kuweza  Kuibua  Masuala Yaliyojificha na Yaliyosahaulika  Ili Kuleta Maendeleo Kwa Jamii  na Kuacha Kuandika Habari za Warsha na Makongamano Kwa Kiasi Kikubwa .

Rai Hiyo Imetolewa na  Bwana Frank Leonard Wakati Akitoa Mafunzo  Siku Mbili Kwa Waandishi wa Habari wa Kituo cha Uplands Radio , na Kusema Kuwa Waandishi Wengi wa Habari Huandika Habari za Vikao na Semina Badala ya Kuandika Habari Zinazoigusa na Kusaidia Kutatua Changamoto Zinazoikabili Jamii .

Katika Hatua Nyingine Mwezeshaji Huyo Amewataka Wanahabari Kuandika Habari kwa  Kuzingatia Maadili ya Kazi  Yao Ili Kuepusha Madhara ya Yanayoweza Kujitokeza Katika Jamii Ikiwemo Migogoro Katika Nchi na Kufanya Kazi Kulingana na Misingi ya Uandishi wa Habari.

Kwa Upande Wao Washiriki wa Mafunzo Hayo Wamesema Yatawasaidia Katika Utekelezaji wa Majukumu Yao ya Kila Siku na Kuongeza Kuwa Mafunzo Hayo Yamewatoa  Kutokana na Kufanyakazi Kwa Kutumia Mfumo wa Zamani wa Uandishi Habari.

No comments:

Post a Comment