Thursday, November 15, 2012

MWALIMU AWALILIA YATIMA MAKETE



Rai imetolewa kwa mashirika na watu binafsi kuwasaidia watoto yatima wanaosoma katika shule ya msingi Ivalalila wilayani Makete, kama namna mojawapo ya kuwafariji kutokana na watoto hao kupoteza wazazi wao

Rai hiyo imetolewa na mwalimu mkuu wa shule hiyo Bw. Nathan Komba wakati akizungumza na mwanahabari wetu ofisini kwake

Mwl. Komba amesema kati ya wanafunzi 398 wanaosoma shuleni hapo, miongoni mwao 90 ni yatima hivyo wanahitaji faraja kutoka kwa jamii

Akizungumzia watoto hao yatima mwalimu huyo amesema wengi wao mahudhurio shuleni si ya kuridhisha kutokana na sehemu wanazoishi na wakati mwingine siku ya alhamisi ambayo ni ya gulio wengi wao hushindwa kufika shuleni na badala yake huenda kuuza mkaa gulioni ili wajipatie kipato

Amesema hali hiyo hupelekea watoto hao kutofanya vizuri katika mitihani yao kwani wanapitiwa masomo kutokana na kutofika shuleni kuhudhuria masomo, hivyo kuiomba jamii na mashirika mablimbali kuwasaidia waoto hao hasa kwa kuwapatia mahitaji ya shule

Na Hadija Sanga

No comments:

Post a Comment