DURU za Habari kutoka Mkoani Mbeya zinasema Mtangazaji na Mwandishi Habari wa Redio BOMBA FM Clemence Mpepo amefariki dunia.
Taarifa kutoka chanzo
chetu zinasema Mpepo amefariki dunia wakati akipewa matibabu katika Hospitali
ya Muhimbili.
Kwa mujibu wa Taarifa
iliyotolewa na Meneja wa Kituo hicho cha Redio Freddy Herbet imesema ni kweli
mpendwa wao amewatoka na juhudi za mazishi zinaendelea kufanyika.
Mtangazaji huyo miezi
miwili iliyopita alifunga pingu za maisha. Alizaliwa Desemba 17, 1980
Katika fani yake ya
Utangazaji alikuwa mahiri kabisa katika Kipindi cha Makabila kilichokuwa
kikirushwa katika redio hiyo na hivyo kujizolea umaarufu hata kufikia kuitwa “MZEE
WA MAKABILA”
No comments:
Post a Comment