
Shamba la mikonge katika kijiji cha Singila, eneo la Mwatate. Mwalimu mkuu wilayani Mwatate alijiua siku ya kwanza ya muhula wa pili Jumatatu. Picha/MAKTABA
Na KENYA NEWS AGENCY
(
email Mwandishi)
Imepakiwa - Tuesday, May 8
2012
at
10:54
Kwa Mukhtasari
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Mwandala,
Taita Taveta alijifungia ndani ya afisi yake na kujinyonga siku ya
kwanza ya muhula. Baada ya matokeo ya KCPE, alikuwa amezomewa na
kufurushwa nje ya shule na wazazi waliokuwa na hasira kutokana na
matokeo mabaya. Haijabainika nini hasa kilimfanya ajitoe uhai.
MWALIMU Mkuu wa shule ya msingi ya Mwandala, wilayani
Mwatate, Kaunti ya Taita Taveta, alijiua baada ya kujifungia ndani ya
afisi yake, siku ya kwanza baada ya shule kufunguliwa kwa muhula wa
pili.
Mwili wa Bw Peter Mwabili
ulipatikana ukining’inia kwenye paa na walimu waliokuwa waliovunja
mlango waweze kuingia ndani ya afisi yake.
Polisi wakiandamana na viongozi
wa eneo hilo, waliwasili baadaye na kuuchukua mwili huku wakiwaacha
wakazi, walimu na wanafunzi wakiwa wameshangazwa na kushtushwa mno na
tukio hilo.
Marehemu aliacha barua
iliyoelezea jinsi ambavyo mali yake ilistahili kugawanywa kati ya wanawe
na mkewe. Alisema mkewe anafaa kurithi robo ya mali huku watoto wake
wanne wakipata thumni (sehemu moja kati ya nane), huku kitinda mimba
akipata sehemu moja kati ya 16 ya mali yake.
Barua hiyo pia iliwataja watu aliokuwa akiwadai na kiasi cha pesa anazowadai na kuwataka walipe madeni kwa familia yake.
Mapema asubuhi
Mkuu wa tarafa ya Mwatate, Bw
Aswani Were, alisema Bw Mwabili alifika shuleni mapema asubuhi Jumatatu
na kujifungia ndani ya afisi yake kabla ya kujitoa uhai.
“Alifika kazini kama kawaida na
kujifungia afisini mwake. Walimu wengine waliompata walilazimika kuvunja
mlango kwani alikuwa amejifungia kutoka ndani,” akasema.
Marehemu alikuwa na wakati mgumu
katika shule ya Mwandala huku wazazi wakati mmoja wakimfurusha na
kumfungia nje ya shule mwishoni mwa mwaka jana wakiitisha kuhamishwa
kwake kutokana na matokeo duni ya Mtihani wa Kitaifa wa Darasa la Nane
(KCPE).
Alikuwa amehudumu kwa muda mrefu
kama mwalimu mkuu katika shule za eneo hilo, ikiwa ni pamoja na shule za
msingi za Kamutonga na Mwachabo kabla ya kuhamishiwa Mwandala kutoka
shule ya msingi ya Mwandisha ambapo alikuwa akihudumu kama naibu mwalimu
mkuu.
Mkuu wa polisi wa kituo cha Taita
Charles Kibet alisema mwili ulipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti cha
Wesu kusubiri kufanyiwa upasuaji.
“Uchunguzi umeanzishwa kuhusu
kisa hicho,” akasema. “Tunajaribu kuchunguza tubaini ni nini huenda
kilimfanya ajitoe uhai,” akasema Bw Kibet.
No comments:
Post a Comment