MIRADI YA MAENDELEO YA MABILONI YA FEDHA YAZINDULIWA NA MWENGE WA UHURU MAKETE
Mwenge wa uhuru ukiwa eneo la mkesha Mabehewani wilayani hapa
Miradi tisa yenye thamani ya zaidi ya
shilingi bilioni mbili imezinduliwa na mwenge wa uhuru ambao unaendelea
na mbio zake katika wilaya ya Makete
Hayo yamebainika baada ya miradi hiyo
kuzinduliwa rasmi na mwenge huo wa uhuru ambapo mkurugenzi mtendaji wa
halmashauri ya wilaya ya Makete Bi Imelda Ishuza amewaeleza maelfu ya
wakazi wa Makete waliofurika katika viwanja vya Mabehewani wilayani Hapo
kuupokea mwenge huo ambao pia utakesha hapo
Akitoa taarifa hizo Bi Ishuza ameitaja
miradi hiyo iliyozinduliwa na Mwenge huo wa uhuru kuwa ni pamoja na
Ofisi ya kijiji kipya cha Ikovo, kituo cha CTC kilichopo ndani ya Kituo
cha afya Matamba, Nyumba bora ya Nuhu Ngogo iliyopo Matamba na Hoteli ya
Kitulo iliyopo Matamba
Mingine ni Vyumba vya madarasa na nyumba
ya mwalimu mkuu shule ya msingi Manga, Mradi wa maji katika kijiji cha
Nkenja, shamba la miti katika kijiji cha Ivalalila pamoja na nyumba tatu
za watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Makete
Akizungumza na wakazi wa Makete kiongozi
wa mbio za mwenge kitaifa Kapteni Honest Ernest Mwanosa amewataka
wananchi kuhakikisha wanaitunza miradi hiyo hasa mradi wa maji, ambao
kwa kiasi kikubwa utawahudumia wananchi wenyewe
"Unajua wananchi utunzaji wa vyanzo vya
maji ni kitu muhimu sana, wilaya ya Makete ni miongoni mwa wilaya chahe
zilizojaliwa kuwa na vyanzo vingi vya maji, tujiepushe kulima kwenye
vyanzo vya maji pamoja na kuendesha shughuli za kibinadamu katika vyanzo
hivyo na badala yake tuvitunze" alisema Mwanosa
Pia amewataka wananchi wa Makete
kujitokeza kushiriki katika mchakato wa katiba mpya kwa kutoa maoni yao
pamoja na kushirikkikamilifu katika sensa ya watu na makazi
itakayofanyika nchi nzima Usiku wa kuamkia Agosti 26 mwaka huu
Mwenge wa uhuru upo wilayani Makete na
kesho utakabidhiwa katika wilaya ya Njombe, na kaulimbiu ya mwaka huu ni
sensa ni msingi wa maendeleo yetu mwananchi shiriki kikamilifu Agosti
26 2012, mabadiliko ya katiba toa maoni
No comments:
Post a Comment