Tuesday, August 13, 2013

NMB TUKUYU WALALAMIKIWA KUSHAWISHI RUSHWA





Na, Gordon Kalulunga, Mbeya
BENKI ya NMB tawi la Tukuyu wilayani Rungwe mkoani Mbeya, imelalamikiwa kuwashawishi kutoa rushwa wajasiliamali wanaohitaji mikopo katika tawi hilo.

Wakizungumza namwandishi wa  blog  hii  wajasiliamali hao walisema kuwa wamekuwa wakikopa na kurejesha vema mikopo yao lakini tangu May mwaka huu, wamezuiliwa na uongozi wa benki hiyo.

Mjasiliamali Habakuki Mbwilo, alisema yeye mwaka jana alikopa 3 Milioni na kurejesha kwa riba ya Shilingi laki tatu na elfu Hamsini, lakini kwa sasa amezuiliwa pamoja na wenzake kwa madai kuwa akaunti yake haina mzunguko mzuri wa fedha.

‘’Mfano ukitaka kukopa Milioni tatu, unaambiwa kuwa unatakiwa uwaachie Shilingi Laki tano lakini deni lako linakuwa pale pale jambo ambalo tunashindwa, hatuna kwa kukimbilia na tunaiomba serikali iingilie kati jambo hili’’ alisema Mbwilo.

Alisema hali hiyo imekuwa kero hata kwa baadhi ya watumishi wa kitengo cha mikopo cha benki hiyo ambao alisema kuwa nao wanasema hawana namna ya kuwasaidia wajasiliamali hao kutokana na maagizo ya meneja wao ambaye amebakiza miaka michache kustaafu.

‘’Hatujawahi kuchelewesha kurejesha wala kukiuka masharti ya mkataba wa mkopo lakini wameamua kutufungia, hatujajua kama labda sera ya serikali imebadilika’’ walisema wajasiliamali hao.

Tanzania daima liliwasiliana kwa njia ya simu na Mkuu wa wilaya ya Rungwe Crispin Meela ambaye alisema kuwa hakuwa na taarifa hiyo.

‘’Sijapata malalamiko hayo lakini  nawaomba kama wanayo malalamiko hayo waje nitashughulikia haraka iwezekanavyo….’’ Alisema Meela.

Wajasiliamali hao wanaolalamikia benki hiyo ni pamoja na wanaofanya biashara za urembo, viatu na vipodozi katika mji wa Tukuyu.

No comments:

Post a Comment