Tuesday, July 30, 2013

Vijina wa Kikristo Mbeya wa ahidi kutaja wauza “Unga” nchini.

 
Mwanafunzi U.D.S atoa ushuhuda jinsi anavyo tumiwa kuzisafirisha
 
MUUNGANO  Vijana wa madhehebu ya kikristo Mkoani Mbeya,wametishia  kutangaza  na kuweka hadharani majina ya mapapa wanaojihusisha na biashara ya  madawa ya kulevya hapa nchini.
 
Tamko hilo limetolewa juzi na  Muungano wa vijana wa kikristo wakati kongamano la   kuhubiri injili na kuliombea taifa mkoani  Mbeya lililofanyika katika kanisa la  Tanzania Assemblies  of   God  Calvary Temple lililopo eneo la Uyole Jijini hapa sambamba  kupinga na kupiga vita matumizi ya madawa ya kulevya kwa vijana kwa kuwa ndiyo waathirika wakubwa na madawa hayo.
 
Akizungumza na Tanzania daima katika viwanja vya kanisa hilo Mchungaji Williamu Mwamalanga wa kanisa la  Pentekoste alisema kuwa vijana wa madhehebu hayo  wameamua kufanya kongamano hilo ili kuishinikiza  serikali ili kuchukua hatua dhidi ya wauza madawa.
 
Alisema kuwa endapo serekali haita chukua hatua dhidi ya vigogo wanao jihusisha na biashara hiyo haramu, vijina hao walisema wapo tayari kuanika majina ya watu maarufu wanao fanya biashara hiyo ambayo ni hatari kwa amani, utulivu na usalama wa nchi.
 
Mchungaji Mwamalanga alisema kuwa biashara ya madawa ya kulevya ni uvunjifu wa haki, na  nchi imepoteza amani kwa kuwa dawa za kulevya zimewafavya vijana wengi wa kitanzania kupoteza haki na uzalendo kwa taifa lao
 
‘Vijana wameamua kuliombea taifa ili kuwarudisha vijana katika kumrudia mungu pia,vijana wamesema kuwa wanatoa siku saba kwa vigogo kuacha tabia ya kuingiza dawa za kulevya hapa nchini ambapo limekuwa janga kwa taifa’ Alisema Mchungaji Mwamalanga.
 
Mbali na kutaja majina ya mapapa wa madawa ya kulevya hapa nchini walisema kuwa wapo tayari kuzitaja  baadhi ya nchi ambazo zinaonyesha kushirika katika biashara ya  madawa ya kulevya na kwamba balozi zote zitapatiwa majina ya vigogo hao.
 
Alisema serikali inatakiwa kuchukua hatua za haraka kwa mapapa hao ambao wamekuwa wanatumia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl Nyerere kama sehemu ya kupokea na kuyapitisha madawa ya kulevya bila kudhibiti hali hiyo inapelekea serikali itapoteza heshima kimataifa.
 
Katika kongamano hilo lililo kuwa na kauli mbiu ya “haki inalinua taifa” mwanafunzi wa  chuo kikuu cha Dar-es-salaamu   mwaka wa tatu alitoa ushuhuda wa jinsi alivyo kuwa akitumiwa na baadhi ya wafanyabiasha  hapa nchini  kusafirisha dawa hizo,sambamba na hilo mwanafunzi (jina tunalo) aliamua kusalimisha  Kg (5)  tano za madawa ya kulevywa aina ya Heroine ambazo alikuwa ameingia nazo Mkoa Mbeya kutoka Jijini  Dar-es-salaamu kwa ajili kuingiza sokoni.
 
Baada ya kupokea dawa hizo mchungaji Mwamalanga kwa kushikiana na waumini walishiriki kongamano hilo waliamua kuzitupa chooni karibu na kanisa hilo alisema kuwa walichukua uamuzi wa kuzitupa chooni bila kuwa shirikisha Jeshi la polisi kutokana na kukosa imani na jeshi hilo..
           

No comments:

Post a Comment