Thursday, June 6, 2013

KAMUHANDA AHAMISHIWA DAR NAFASI YAKE YASHIKWA NA ACP RAMADHANI MUNGI






Aliyekuwa kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Kamuhanda




Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP, Saidi Mwema, amemhamishia makao makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda.

 Kamuhanda anakumbukwa kwa kusimamia operesheni ya jeshi hilo mkoani Iringa dhidi ya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliokuwa wakifungua tawi la chama hicho katika kijiji cha Nyololo Septemba 2 mwaka jana katika operesheni hiyo mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Chanel Ten, Daudi Mwangosi, aliuawa na bomu lililodaiwa kutoka kwa mmoja wa askari waliokuwa wakimdhibiti mwandishi huyo.


 Kutokana na mabadiliko hayo nafasi ya Kamuhanda imechukuliwa na ACP, Ramadhan Mungi (aliyekuwa Makao Makuu ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai).

 Katika taarifa ya Jeshi la Polisi kwa vyombo vya habari, mbali na Kamuhanda, makamanda wengine waliohamishwa ni ACP Charles Kenyela (RPC Kinondoni) aliyehamishiwa makao makuu ya upelelezi wa makosa ya jinai.

 DCP, Ally Mlege, aliyekuwa Makao Makuu ya Polisi amehamishiwa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na kuwa mkuu wa utawala na rasilimali watu.

 ACP Duwani Nyanda aliyekuwa makao makuu ya idara ya upelelezi amehamishiwa mkoani Arusha kuwa mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai.

 Taarifa hiyo imeeleza kuwauhamisho huo ni wa kawaida kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Jeshi la Polisi.

No comments:

Post a Comment