Thursday, March 14, 2013

WALIMU LUDEWA WATAKIWA KULIPIA NYUMBA WANAZOISHI ILI KUONGEZA PATO LA HALMASHAURI.


Na Bazil Makungu Ludewa


WAKATI watanzania, wazazi, wadau mbalimbali wa elimu na taifa wakitafakari juu ya kutoa motisha na kutengeneza mazingira mazuri kwa walimu ili waweze kufundisha na kuishi katika mazingira magumu hasa vijijini, madiwani katika halmashauri ya wilaya ya Ludewa katika Mkoa wa Njombe wao wamewataka walimu wanaoishio kwenye nyumba za serikali kuanza kulipia pango mara moja.

Maagizo hayo ya madiwani katika halmashauri ya wilaya ya Ludewa imekuja muda mfupi huku taifa likihangaika na kuunda tume ya kubaini na kumtafuta mchawi yupi aliyehusika na matokeo mabovu ya mtihani wa kidato cha nne mwaka huu.

Kwa mujibu wa barua zilizosambazakwa walimu wakuu ambazo nakala tunayo, walimu wote wanatakiwa kulipia nyumba hizo kwa kiwango cha shilingi elfu(10,000) bila kujali ubora wala uimara wa nyumba hizo na haijalishi kama nyumba hiyo imejengwa kwa kutumia miti, nyasi, bati au saruji kila anayeishi kwenye nyumba ya serikali pasipo kujali kama nyumba hiyo iko mjini au kijijini atatakiwa kulipia pango.

Wakizungmza na gazeti hili kwa nyakati tofauti walimu wa shule za sekondari na msingi wameeleza kusikitishwa kwao na maamuzi ya madiwani yakuwatoza kodi bila kuangalia uborawa nyumba zenyewe na kuongeza kuwa kuna nyumba hazifai kuishi binadamu lakini wao wanavumilia.

Aidha wamesema kuwa wapo wanaokatwa kodi lakini hawaishi kadhaa, ubabe unaofanywa na madiwani katika halmshauri ya wilaya ya Ludewa hasa katika masuala mbalimbali bila kuwahusisha wataalamu waliokaa muda mrefu darasani kupata taaluma zao.

Akijibu malalamiko  ya walimu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa Matei Kongo alisema kodi hiyo inawahusu watumishi wote ndani ya wilaya yake wakiwemo idara ya elimu na afya ili mradi awe anaishi katika nyumba ya serikali ikiwemo zile nyumba zilizojengwa kwa mpango wa MAM na MES watalazimika kulipia.

‘’’’’ hakuna mkataba wowote tuliokubaliana na watumishi kwamba wanapoletwa kuanza kazi lazima tuwajengee nyumba, mtumishi aliomba kazi na kuingia mkataba na serikali kisha kuletwa Ludewa kwa ajili ya kufanyakazi kama ajira yake invyosema na si kuishi bure kwenye nyumba yetu.’’’’’’ Alifafanua Kongo

Tuwe na wazo la pamoja la kuendeleza nyumba zetu kwa hiyo kila mwalimu anayeishi kwenye nyumba ya serikali  achangie gharama ya hiyo nyumba ili ikiwezekana tukikusanya kwa mwaka tuweze kujenga nyumba zingine mahali pengine kwa sababu halmashauri inatakiwa kujitegemea.

Tulitoa wazo nyumba tukaziangalia kwanza zile ambazo ni za kati walimu walipe shilingi elfu tano lakini zile ambazo zipo kwenye mpango wa MEM na MES zilipiwe 10,000 na kwa zile ambazohazifai kabisa wakae bure kwa sababu zipo katika hali nzuri.

‘’’’’ mtumishi wa kawaida anaishi kwenye nyumba na kulipa shilingi elfu kumi na tano mpaka ishirini lakini sisi tunatoza kiwango cha juu 10,000 hawawezi kushindwa kulipia.’’’’ Alisisitiza Kongo

‘’’’’ ukiwa mtumishi una mkataba wko ni suala la mwajiri kukupa motisha lakini kulingana na uwezo hakuna mkataba wa kutoa nyumba bure huo ni mchangokwa mtumishi na halmashauri ili tuweze kufanya ukarabati wa nyumba hizo.’’’’ Akaongeza kongo

Aidha mwenyekiti huyo alimtaka afisa elimu msingi kuliangalia upya tangazo lililobandikwa katika ubao wa matangazo likiwataka walimu kupeleka shida na matatizo yao siku ya ijumaa pekee.

Akaongeza kuwa watumishi na watu wengine wanataka kupatiwa huduma mara zote na wakati wowote sasa unapowapangia siku moja idadi ya watu zaidi ya mia mbili inageuka kero.
mwisho


No comments:

Post a Comment