Friday, March 15, 2013

DIWANI MAKETE KORTIN KWA TUHUMA ZA KUGUSHI SAHIHI NA KUIBIA SERIKALI ZAIDI YA MILIONI 2



 Watu wawali wa wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya makete kujibu tuhuma za kugushi sahihi na kuandika mhutasari katika kikao hewa na kuchukua zaidi ya shilingi milioni mbili katika akaunti ya mfuko wa maendeleo wa kata ya bulongwa

Akitoa taarifa hiyo kwa wanahabari ofisi kwa kwake mwendesha mashitaka wa PCCB bwana Frednandi Nsakuzi amewataja watuhumiwa hao kuwa ni aliye kuwa diwani wa kata ya Bulongwa Estomin Mahenge na mwenzake Edwin swallow ambaye alikuwa mtendaji wa kijiji mpaka anafanya tukio hilo alikuwa anakaimu ofisi ya mtendaji wa kata ya Bulongwa

watuhumiwa hao waligushi sahihi na kuandika mhutasari wa kikao hewa na kwenda katika benki ya Nmb na kuchukua zaidi ya shilingi million mbili kwenye akaunt ya mfuko wa maendeleao ya kata ya Bulongwa wakidai kuwa ni kwajili ya ujenzi wa shule ya sekondari Usililo ambapo  mhutasari huo ulikuwa  baadaye ya taasi ya kupambana na


Watuhumiwa hao walifikishwa mahakamani  hapo jana  na walikana mashitaka yanayowakabili kesi hiyo inatarajiwa kutaja tena  tarehe 23 mwezi wa 3 mwaka huu katika mahakama wilaya makete
  
Aidha katika hatua nyingine mkurugenzi wa Pccb wilayani Makete bwana Daudi Ndyamkama amewahasa wana makete kushilikiana na taasisi hiyo pindi wanapokuwa na kesi kama hizo hususani inapokuwa katika hatua ya ushaidi mahakamani bwana ndyamkama amesema kumekuwa na vitendo kama hivi katika vijiji vingi wilayani hapa lakini wananchi wamekuwea hawatoi ushilikiano katika kesi hizo pindi wanapo hitajika kutoa ushahidi mahakamani na badhi yao wamekuwa wakirubuniwa na watuhumiwa

No comments:

Post a Comment