Leo taarifa ambayo metrend vya kutosha kwa muda mfupi, ni kuhusu
Rais wa J.M wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kutengua uteuzi wa
aliyekuwa mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mama Anne Kilango Malecela katika
nafasi hiyo.
Mwanasiasa huyu Mkongwe amekumbwa na Panga hili baada ya kutoa
taarifa hadharani kuwa, Mkoa wa Shinyanga haukuwa na watumishi hewa.
Kauli ambayo ilikinzana na tume rasmi ya uchunguzi iliyotumwa mkoani
humo, ambapo iligundua watumishi hewa 45 na bado uchunguzi Zaidi
unaendelea.
Sasa Mtangazaji wa Sun Rise, Stanslaus Lambert, amezungumza kwa simu
na Mbunge huyu wa zamani wa Same Mashariki ambapo amedai yeye hana
taarifa ya utenguzi wake kutoka kwa Rais.
“Jamani Mimi sina taarifa sipendi kukizungumzia maana yake sijaambiwa
na aliyeniteua, sina la kukwambia.” Alisema na kukata simu.
Anne Kilango Malecele amedumu kwenye nafasi hiyo kwa majuma kadhaa, hata mwezi mmoja hajafikisha.
No comments:
Post a Comment