Thursday, September 17, 2015

UN;BURUNDI BADO KUGUMU



Vikosi vya BurundiMchunguzi maalum wa
umoja umataifa anaonya kuwa Burundi huenda ikatumbukia tena kwenye vita, kama jumuiya ya kimataifa haitachukua hatua za haraka  kuzuia hilo.
Pablo de Greiff, mchunguzi  maalum wa umoja mataifa kwa ukiukaji mkubwa, anasema mengi yametokea  tangu alipoitembelea Burundi mwezi December, na hamna lilo zuri. Anasema ,Burundi imejiondoa kwenye  njia ya amani ambayo imeifuata tangu mwaka 2000, pale makubaliano ya Arusha yalipomaliza  vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.

Anasema serikali ya rais Pierre Nkuruzinza haijaribu tena kujenga jamii kutokana na kanuni za sheria, na kwamba  utamaduni wa kutokhifia  kushtakiwa kutoka miongo iliyopita  umejikita zaidi  na unatumiwa  kama nyenzo ya ukandamizaji na ghasia.
De Greiff anasema amewasilisha wasiwasi wake kwa baraza la haki za binadam la umoja mataifa kwa matarajio nchi  kuwa nchi wanachama  watafahamu  ukubwa  wa hali inayojitokeza  nchini Burundi na kuchukuwa hatua ili kuepuka  janga kutokea.
 De Grieff anasema, anataka kuwa muwazi, na kujaribu kutowa wito wa haraka na wito wa tahadhari  kwa jumuiya ya kimataifa, wasisubiri hadi tufikwe na janga jingine mikononi mwetu kabla ya kuchukuwa hatua.
Takriban watu laki 3 waliuwawa  wakati wa vita vya wenyewe kwa  wenyewe nchini Burundi.
Taifa hilo lilikuwa na Amani katika miaka ya karibuni hadi mwishoni mwa mwezi Aprili, pale rais Nkuruzinza alipotangaza kuwania muhula wa tatu madarakani. Tangu wakati huo, De Greiff anasema, kumekuwepo  na Zaidi ya mauwaji mia 1, mamia ya ukamataji  holela na kesi nyingi za mateso na kutendewa vibaya.
Anasema hamna kesi inayochunguzwa ila moja inayohusisha afisa wa serikali.
 Rais alichaguliwa tena mwezi July, lakini mivutano bado ipo baina ya wafuasi wake na wale wanaosema amekiuka katiba ambayo imeweka kiwango cha mihula miwili tu kwa rais kuwepo madarakani.
Mchunguzi huyo wa umoja mataifa anasema jumuiya ya kimataifa na serikali za kikanda haziwezi kumudu kukaa  na kusubiri ukatili mpya utokee  tena nchini  Burundi. Anaonya kuwa hii inahatarisha mzozo mkubwa kuweza kutokea katika  eneo la  maziwa makuu, na matokeo ambayo yanatisha na yasiyojulikana.

1 comment: