Monday, May 25, 2015

JK ACHAGUA MKUU WA WILWYA MMOJA AHAMISHA 10

Raisi Jakaya Kikwete

Rais Jakaya Kikwete amemteua Anthony Peter Mavunde kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Mkoa wa Dodoma, kuanzia jana.
 
Aidha, Rais Kikwete amefanya uhamisho wa wakuu 10 wa wilaya kwa nia ya kuongeza ufanisi katika uongozi wa Wilaya mbali mbali nchini.
 
Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu ilieleza kuwa, katika mabadiliko hayo, Rais Kikwete amemhamisha Luteni Edward Ole Lenga kutoka Wilaya ya Mkalama, Mkoa wa Singida kwenda kuwa mkuu wa wilaya mpya ya Kyerwa, Mkoa wa Kagera. Luteni Lenga anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Luteni Kanali Benedict Kulikela Kitenga ambaye alifariki dunia Aprili 20, mwaka huu, 2015.
 
Wakuu wengine wa wilaya waliohamishwa ni Elizabeth Chalamila Mkwasa kutoka Wilaya ya Dodoma kwenda Wilaya ya Mvomero, Mkoa wa Morogoro; Dkt Jasmine Tisike kutoka Wilaya ya Mpwapwa kwenda Wilaya ya Dodoma; Agnes Elias Hokororo kutoka Wilaya ya Namtumbo, Mkoa wa Ruvuma kwenda Wilaya ya Tunduru, mkoani humo humo na Fadhili Nkurlu kutoka Wilaya ya Misenyi, Mkoa wa Kagera kwenda Wilaya ya Mkalama.
 
Wengine ni Chande Bakari Nalicho kutoka Wilaya ya Tunduru kwenda Wilaya ya Namtumbo; Festo Shem Kiswaga kutoka Wilaya ya Mvomero kwenda Misenyi; Darry Ibrahim Rwegasira kutoka Wilaya ya Karagwe, Mkoa wa Kagera kwenda Wilaya ya Biharamulo, mkoani humo humo; Elias Choro John Tarimo kutoka Wilaya ya Biharamulo kwenda Chunya, Mkoa wa Mbeya na Deodatus Lukas Kinawiro kutoka Wilaya ya Chunya kwenda Wilaya ya Karagwe, Mkoa wa Kagera.

No comments:

Post a Comment