
Dar es Salaam. Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda amesema alichanganyikiwa kiasi cha kushindwa kujielewa kwa muda baada ya kupigwa risasi.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mwananchi
kwenye wodi binafsi ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (Moi)
alikolazwa jana, Sheikh Ponda alisema kutokana na hali hiyo hakumbuki
matukio yaliyofuata baada ya hapo.
“Sikumbuki hata nilipata huduma ya kwanza
hospitali gani kwa sababu sikuwa katika hali ya kawaida. Mambo mengine
yaliyotendeka kabla ya kujeruhiwa ninayakumbuka vizuri,” alisema Ponda
ambaye inasadikiwa kwamba alipigwa risasi ya begani, Ijumaa iliyopita
mjini Morogoro.
Alisema alihutubia katika Kongamano la Waislamu
kwa muda mfupi akizingatia muda uliokuwa umetolewa kumaliza mkutano huo
na baada ya hapo alishuka na kupanda kwenye gari binafsi ambalo
lilizingirwa na polisi ndipo akaamua kushuka na kuanza kutembea kabla ya
kujeruhiwa.
Mahojiano maalumu na Sheikh Ponda
Swali: Je, watu waliokupa huduma ya kwanza mara baada ya kujeruhiwa walikuta risasi iliyokujeruhi?
Jibu: Nilipigwa risasi kwa nyuma ikatokea mbele
kwa hiyo haikubaki mwilini wala haikuonekana ilipoangukia kwa wakati huo
maana kulikuwa na purukushani.
Swali: Ulipata wapi huduma ya kwanza?
Jibu: Kwa kweli kwa sasa siwezi kukumbuka
nilihudumiwa wapi kwa sababu mara baada ya kujeruhiwa sikuwa katika hali
yangu ya kawaida, nilichanganyikiwa.
Swali: Utathibitisha vipi kama ulipigwa risasi?
Jibu: Bahati nzuri ni kwamba tukio hili lilitokea
kweupe wapo wengi walioshuhudia, kwa hiyo wanaweza kusaidia kuthibitisha
na ushahidi mwingine ni jeraha hili.
Swali: Nini msimamo wako baada ya tukio?
No comments:
Post a Comment