Tuesday, November 13, 2012

MAMLAKA YA MAJI MAKETE YAFANYA KWELI



 chanzo cha maji Ivalalila

 Mmoja ya wafanyakazi ya maji wakipanda miti aina ya miturunga pembezoni mwa chanzo cha maji

Mamlaka ya maji katika mji wa Iwawa imeanza mikakati ya kuboresha huduma hiyo ili kuondokana na shida ya upatikanaji wa maji kwa watumiaji wa huduma hiyo.

Akizungumza na kitulo fm meneja wa maji mjini hapa bwana Jornas Ndomba amesema kuwa tayari wameshanza  jitihada za kuongeza kingo za pembeni katika chanzo kikuu cha mji kilichopo Ivalalila kwaajili kuzuia maji mengi ili kutopungukiwa na maji hususani wakati wa kiangazi ambapo maji hupungua na kutojitoshereza jambo ambalo lina leta kero kwawatumiaji wa huduma hiyo. 

Sambamba na hilo pia mamlaka ya maji imepanda miti aina ya miturunga kuzunguka eneo la chanzo hicho cha maji kwa ajili ya kuendelea kuongeza maji kwa wingi katika chanzo hicho .

Katika hatua nyingine bwana Ndomba amewaomba wakazi wa Ivalalila kukitunza chanzo hicho kwa kutoendeleza shughuli za kibinadamu katika chanzo hicho kwani kuna baadhi ya watu wamekuwa na tabia ya kufanya shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo ufungaji na upandaji wa miti bila kuzingatia sheria za ardhi jambo ambalo linasababisha uhaba wa maji mjini hapa

No comments:

Post a Comment