Uongozi wa Mamlaka ya Mji mdogo wa Bunda, umeipa hospitali teule
ya wilaya hiyo siku tatu ya kuhakikisha kuwa mazingira yake yanakuwa
katika hali ya usafi, vinginevyo itasimamishwa kutoa huduma kwa jamii.
Hatua hiyo imefikiwa jana na uongozi huo baada ya
kufanya ziara ya kushtukiza katika hospitali hiyo na kushuhudia
mazingira machafu hasa vyooni na wodini huku maji machafu yakitiririka
hovyo kutoka vyooni na mahala pa kufulia kuelekea kwenye makazi ya
watu.
watu.
Wakiongea kwa nyakati tofauti hospitalini hapo,
viongozi wa mamlaka hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti Pastory Ncheye na
Ofisa mtendaji wake Charles Machage wamesema , mazingira ya hospitali
hiyo yanatia shaka kuhusu huduma za matibabu zinazotolewa mahala hapo
hivyo wameutaka uongozi wa hospitali kuyasafisha mazingira yake
vinginevyo itaisimamisha kufanya kazi.
Akisisitizia hilo Ncheye amesema inatia aibu kuona
kuwa hospitali ambayo inaelimisha watu namna ya kujikinga na magonjwa
pamoja na kuwatibu pindi wanapougua mazingira yake ndiyo yanayoongoza
kwa uchafu wenye kuchangia maambukizo ya maradhi kwa jamii jambo
linalotia shaka kama kweli hospitali hiyo inawiwa na afya za watu.
“Jamii inategemea kuyaona mazingira ya hospitali
katika hali ya usafi lakini kwa hapa hali ni kinyume.Sasa tunawataka
muisafishe hospitali yenu ndani ya siku tatu vinginevyo tutawazuia kutoa
huduma,”aliseman Ncheye.
Hata hivyo Ncheye ametilia shaka utendaji kazi wa
wataalamu wa idara ya afya wenye jukumu la kuangalia hali ya usafi ndani
ya mamlaka hiyo kama wanatekeleza majukumu yao vizuri kwani hawajawahi
kuitolea taarifa yoyote hospitali hiyo kuhusu mazingira yake na
kumwagiza ofisamtendaji wa mamlaka hiyo kuwachunguza na kuwachukulia
hatua ikibainika kama walizembea katika hilo.
Kwa upande wake katibu wa hospitali hiyo, Billy Kinyaha alipoulizwa alikiri kuwepo kwa hali ya uchafu hospitalini hapo unaosababishwa na
Kwa upande wake katibu wa hospitali hiyo, Billy Kinyaha alipoulizwa alikiri kuwepo kwa hali ya uchafu hospitalini hapo unaosababishwa na
ukata unaoikabili kutokana na Serikali kutoipatia
fedha za uendeshaji kwa wakati na kusema wanajitahidi kuyasafisha kwa
fedha kidogo wanazozipata kutoka katika chanzo ambacho hakukitaja na
kwamba kwa sasa hali ya usafi inaendelea kuboreka.
No comments:
Post a Comment