Thursday, July 5, 2012

Chama cha mapinduzi wilayani makete kimepongeza tamko la Rais kuhusu mgomo wa madaktari

NA RIZIKI MANFRED BONZUMA                                                                                                                                                         5/6/2012
MAKETE

Chama cha mapinduzi  wilayani makete kimepongeza tamko la Rais kuhusu mgomo wa madaktari alilolitoa kupitia hotuba yake ya mwishoni mwa mwezi jun mwaka huu
                             akizungumza na kwanza jamii kwaniaba ya chama cha mapinduzi katibu wilaya  ya makete bwa Mlaji mtaturu amesema kuwa anapongeza hatua aliyo ichukua rais wa jamhuri  ya muungano waTanzania mheshimiwa Jakaya Mlisho Kikwete kwakuwataka madaktari kurudi kazini haraka iwezekanavyo kwani kufanya hivyo kumenusuru maisha ya wengi kwani mgomo huo ulikuwa ukiwalenga zaidi wananchi wa hali ya chini hivyo kwa tamko la Rais amewakomboa  watanzania
       Aidha bwana Mtaturu ametumia muda huo kuwapongeza madaktari wa wilaya Makete kwa kutoshiriki katika mgomo huo licha ya madaktari wasehemu zingine kuendea kushinikiza mgomo huo karibu nchi nzima lakini hali ilikuwa tofauti''nawashukuru madkitari wa makete kwakutojiingiza katika mgomo huu na kundelea kuwahudumia wagonjwa jambo ambalo linaijengea heshima wilaya Makete ''alisema Mtaturu na kuongeza kuwa jambo la kuigwa kwa madaktari wengine nchini kwani kwa kufanya hivyo unalijengea heshima taifa la Tanzania
             akiendelea bwana Mtaturu ameungana na watanzania wengine kutoa pole kwa dk Ulimboka kwa kitendo alichofanyiwa ambacho amekiita sio cha kiugwana na kukemea tabia hiyo nakuomba hatua kali zichukuliwe kwa wahusika

No comments:

Post a Comment