Wednesday, July 31, 2013

DODOMA WAASWA KUWAMBALI NA MATAPELI

Dodoma. Polisi mkoani hapa wamewataka wananchi kujiepusha na matapeli ambao wamejitokeza kwa wingi kwa siku za hivi karibuni na kuwatapeli watu wengi.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, David Misime alitoa wito huo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake kufuatia kuibuka kwa wimbi la matapeli mjini hapa.
Alitoa kauli hiyo kufuatia kuwapo kwa matapeli ambao walichukua fedha za watu wengi wakidai watatoa ajira kwa kazi ya kuandikisha watu wanaotaka vitambulisho vya taifa.
Misime alisema watu wanapaswa kupata taarifa sahihi.

No comments:

Post a Comment