Wednesday, March 13, 2013

UNYANYASAJI WAKINJISIA CHANZO CHA KUSHUSHA ELIMU MAKETE


Na Edwin Moshi, Makete
Vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia vinavyoendelea kufanyika kwa wanafunzi wa shule za sekondari wilayani makete mkoani Njombe ni miongoni mwa visababishi vikubwa vinavyochangia wanafunzi kutofikia malengo yao
Hayo yamebainika wakati wanafunzi wa shule ya sekondari Mlondwe ilkiyopo kata ya Itundu wilayani hapo wakizungumza na mtandao huu wakati wa kuandaa vipindi vya redio shuleni hapo kwa ushirikiano na shirika la SUMASESU, ulipotaka kufahamu sababu zinazopelekea wanafunzi kushuka kitaaluma siku hadi siku katika shule za sekondari wilayani Makete
Mmoja wa mwnafunzi aliyejitambulisha kwa jina moja la Sanga ambaye anasoma kidato cha tatu shuleni hapo amevitaja baadhi ya vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia wanavyofanyiwa wanafunzi wawapo shuleni kuwa ni wanafunzi wa kidato cha kwanza kutishiwa, wavulana kunyang’anywa sahani zao wakati wa kula na wanafunzi wa vidato vya juu kwa madai kuwa wao ni watoto wa kiume wanaweza kuvumilia njaa pamoja na vipigo vya mara kwa mara
“Unakuta mwanafunzi anakuita wewe wa form one (kidato cha kwanza) anakunyang’anya sahani yako na ukileta ubishi anaitumia halafua anaipasua, unakuta mimi sina nguvu za kumpiga na pia naogopa kwenda kusema kwa mwalimu sasa hii kwa kweli sidhani kama mwanafunzi ataitamani shule, nia lazima afeli”alisema Sanga
Kwa upande wake Emmy anayesoma kidato cha pili shuleni hapo amesema wapo baadhi ya wanafunzi wa kiume ambao wanakaguliwa na wavulana wa vidato vya juu kama wamedondosha mkono sweta (wamefanyiwa tohara) na endapo itagundulika hawajatahiriwa huambulia kipigo na vitisho, adhabu kutolewa bila usawa na wakati mwingine adhabu kali zaidi, pamoja na wanafunzi kujihusisha kimapenzi na waalimu na wanafunzi wenzao
Awali mratibu wa program ya shule salama kutoka shirika la SUMASESU Bi Anifa Mwakitalima aliwataka wanafunzi hao kutokuwa na woga wa kuvitaja vitendo hivyo wanavyofanyiwa kwa madai ya kuogopa ama kuona kama ni vitendo vya kawaida, na badala yake waseme ukweli ili vitendo hivyo vikomeshwe
“Unaweza kukuta wakati vipindi hivyo vitakapoanza kurushwa redioni watu wengi watasikia wengine vitakuwa vinawalenga, hivyo wengine wataacha na hata serikali ikatatua baadhi ya changamoto ili shule yenu izidi kuwa salama
Shirika la SUMASESU hivi sasa linatekeleza program ya shule salama ambapo pamoja na mambo mengine linaandaa vipindi vya redio ambavyo vinahusiana na shule salama kutoka kwenye maeneo yote ambayo mradi huo unatekelezwa

No comments:

Post a Comment