Wednesday, January 2, 2013

NMB MAKETE YAMWAGA ZAWADI KWA WAGONJWA





Katika kusherekea sikuu ya mwakampya benki ya NMb tawi la Makete  ilitembea katika hospitali ya wilaya ya Makete na kuwaliwaza wagonjwa pamoja na kuwapa zawadi za mwaka mpya .

Meneja wa benki hiyo bwana Anyambilile Ambingile alisema hatua hiyo imekuja baada ya kuona niviziri wakaenda kuwaona wagonjwa ambao wapo katika hospitali hiyo ili kuwapa moyo wangonjwa pamoja na kuwapa zawadi za mwaka mpya jambo ambalo litawafanya waongeze matumaini kuweza kupona na baadaye kiruhusiwa kutoka na wao kama taasisi kuwapa faraja

Adha Ambingile aliyaomba mashirika taasisi  za dini pamoja serikali kuiga mfano huo kwa kuwatembelea mara kwa mara watu kama hao kwani kwa kufanya hivyo kunaleta mahusiano mazuri kati ya jamii na taasisi “tunaomba jamii ielewe kuwa suala la kuwasaidi watu katika jamii ni la kila mtu aliyenacho ndo maana nasema mashika yaige mfano huu ilikujijengea mazingira mazuri na ushikiano mzura baina ya taasisi na jamii kwani kwa kufanya hivyo kutasadia jamii iwe na mtazamo mzuri na kwa taasisi hizo”alisema Ambingile

Kwa upande wake kaimu mganga mkuu wa wilaya Michael Guraka alipongeza kitendo hicho na kuwapongeza benki hiyo kwa kuwakumbuka wagonjwa hao ambao wamekuwa wakikosa furaha hasa katika msimu huu wa sikuu kwani huwa wanakosa liwazo kwaupande wake Rehema Mahenge ambaye alilazwa katika wodi ya wazazi alishukuru kwa uongozi mzima wa benki hiyo kwa kuwakumbuka wagonjwa na kuwaomba kundlea kufanya hayo zaidi katika siku za usoni na wasishi hapo

No comments:

Post a Comment