Mimi na Dada yangu Linah Sanga
"Malkia wa Nguvu" tutashirikiana kwenye Uzinduzi wa Mradi Mkubwa kuwahi
kutokea katika nyanda za juu kusini Mradi wa DREAMS.
DREAMS ni
mradi unaowalenga wanawake vijana wenye umri kati ya miaka 15-24 wenye
nia ya kuwajengea uwezo wa kukabiliana na changamoto zinazoweza
kuwapelekea kupata maambukizi ya UKIMWI.
Uzinduzi utafanyika Siku ya Mtoto wa Afrika June 16 katika viwanja vya
Ruanda Nzovwe ukitanguliwa na maandamano yatakayoanzia Kituo cha
daladala cha Kabwe. Linah atafanya shughuri nyingi za kijamii ikiwemo
kushiriki semina kadhaa, kufanya mazungumzo na makundi mbali mbali ya
vijana walio nje ya mashule. Atafanya mahojiano kadhaa na redio zilizopo
hapa Mbeya na Kisha kupanda Jukwaani siku ya June 16.
Kwa wanamakete wanaotaka kuonana na Dada Linah waliopo hapa Mbeya tunaweza kutafuta muda jioni tukapiga naye story
taarifa hizi ni kwa mujibu wa
pia mtandao wako wa www.rizikimgaya.blogspot.com utakuletea moja kwa moja yote yatakayojiri katika uzinduzi huo
No comments:
Post a Comment