Monday, February 8, 2016

MWANAMUZIKI PETER WA P-SQUARE ATUHUMIWA KUMSALITI MKE WAKE NA MCHEPUKO WA MAREKANI..SHUHUDIA HAPA


POP staa, Peter Okoye ametuhumiwa kumsaliti mkewe, Lora Omotayo baada ya kuripotiwa kuwa ametoka na modo anayefahamika zaidi kupitia Instagram, Aimee ambaye makazi yake yapo Marekani.
Awali,mrembo huyo aliposti picha kwenye Instagram akiwa na Samuel Eto’o na kusema kuwa yupo kwenye maandalizi ya kurejea London akidai kuwa ndiyo sehemu pekee ukitoa Marekani ambayo anapenda kuishi na wakati huo alikuwa akitokea Paris, Ufaransa kwenye mishe zake.

Peter na Mchepuko wake

Kilichoharibu; baada ya kutupia picha hiyo ambayo ilipigwa na Peter kisha staa huyo naye ‘akashare’ hapo ndipo ishu ikaibuka baada ya mfuasi wao mmoja kukomenti kuwa nyota huyo kutokaKundi la P Square anatoka na modo huyo na amekuwa akizunguka naye miji kama Paris, Antalya na London na kumuacha mkewe nyumbani.

Shabiki huyo ambaye anatumia jina la Mihlany kwenye Instagram,alimwaga mboga kuwa nyota huyo amekuwa akimsaliti mkewe kwa kutoka na modo huyona wiki iliyopita walikuwa pamoja Paris kabla ya kwenda kukutana tena Marekani.

Baada ya komenti hiyo, Peter na modo huyo waliifuta na kumblock kabisaMihlany kwani alishachafua hali ya hewa. Modo huyo alisema: “Tetesi ni burudani lakini wakati mwingine zinawaharibia wahusika.

Kila mmoj ana familia yake na siyo vizuri kunihusisha na mtu mwingine kwani ni rafiki tu na hakuna cha zaidi.”

No comments:

Post a Comment